Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

24 Desemba 2018

UHAMIAJI SACCOS YAWAFARIJI WATUMISHI WAGONJWA NA WASTAAFU WA IDARA YA UHAMIAJI

Kamishna wa Utawala na Fedha Peter Chogero akimsalimia Mkurugenzi mkuu mstaafu wa Idara ya Uhamiaji Rafael Kubaga aliyestafu miaka miaka 30 iliyopita

Mwenyekiti wa Uhamiaji SACCOS akimsalimia Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Uhamiaji Rafael Kubaga wakati walipomtembelea nyumbani kwake Keko jijini Dar es salaam
Kamishna wa Viza Salum Mwichumu aliongozana na Maafisa Utumishi Mjogoro na Nuru Stephen kutembelea watumishi wa Idara ya Uhamiaji ambao ni wagonjwa kwa kuwajulia hali na kuwapatia zawadi ya Krismasi na Mwaka Mpya.
 





Kamishna wa Uhamiaji Utawala na Fedha Peter Chogero, Makamishna wa Uhamiaji Sheria na Viza Hanelore Manyanga na Salum Mwichumu, Mwenyekiti wa Saccos ya Uhamiaji Mrakibu Msaidizi Mdeme Charles, Leo tarehe 24 Disemba 2018 wamewatembelea wagonjwa ambao ni watumishi wa idara ya Uhamiaji pamoja na wastaafu kuwajulia hali zao pamoja na kuwapatia zawadi ya krismasi zilizotolewa na Uhamiaji SACCOS

Kwa niaba ya Kamishna Jenerali na watumishi wote wa idara ya Uhamiaji tumekuja kuwaona ndugu zetu kujua mnaendeleaje na afya zenu  tumekuja kuwapatia zawadi za krismasi na mwaka mpya kwa niaba ya afande Jenerali Anna Makakala ambaye ndio mlezi wa SACCOS kuonyesha bado tuko na ninyi katika kipindi hiki cha ugonjwa”amesema Kamishna Chogero

Aidha Kamishna Chogero amesema Idara ya Uhamiaji ipo pamoja na watumishi waliopo kazini na wastaafu ndio maana Uhamiaji SACCOS imewakumbuka kwa kutoa zawadi ya sikuku ya krismasi ili wafurahie vizuri.

Kwa upande wa Kamishna Mstaafu Dowson Mongi amesema “Namshukuru sana Kamishna Jenerali Anna Makakala kwa upendo anaotuonyesha kwa wastaafu na wagonjwa inaonyesha jinsi gani anatuthamini sie wastaafu,mungu aendelee kuwapa moyo wa upendo watumishi wote wa Idara ya uhamiaji

Pamoja na ziara hiyo ya kuwatembelea wagonjwa Kamishna Chogero na Kamishna Mwinchumu wamewatakia watumishi wote wa idara ya Uhamiaji heri ya krismasi na mwaka mpya.

Aidha amewakumbusha wananchi kutoa taarifa ya Uhamiaji au vyombo vya Dola pale wanapoona watu au makundi ya watu wanaohisiwa kuwa ni wahamiaji haramu hasa katika kipindi hiki cha sikukuu za Krismasi na mwisho wa Mwaka




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni