Visitors
31 Desemba 2019
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Afanya Ziara ya Kushitukiza Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Nyerere. (JNIA)
Dar es salaam
Akifanya Kikao na Watumishi kituoni hapo Dkt.Makakala amewataka watumishi wote wanaofanya kazi katika kituo hicho kufanya kazi kwa nidhamu, utii, uhodari, na weledi na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ikiwemo kutojihusisha na masuala ya rushwa.
Aidha ameapa kutowavumilia maafisa askari na watumishi wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na kwamba atawachukulia hatua kali za kinidhamu ikiwemo kuwafuta kazi na kuwafikisha mahakamani.
Sanjari na hilo amesisitiza pia kuongeza juhudi za ukusanyaji maduhuli ya serikali ili kuongeza pato la taifa na kuchochea maendeleo kwa faida ya kizazi cha sasa na baadae.
Ili kuongeza ufanisi zaidi katika utekelezaji wa majukumu ya ulinzi na usalama wa nchi kupitia mipaka na njia zote za kuingilia na kutokea nchini, Dkt. Makakala amewataka maafisa na askari wote kushirikiana na vyombo vyote vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha nchi inakuwa salama.
Ziara ya Kamishina Jenerali ni muendelezo wa ziara za mara kwa mara katika kukagua shughuli za utendaji kazi ili kuhakikisha idara inafikia malengo yake mahususi ya utendaji kwa kutoa huduma za uhamiaji zenye kukudhi viwango vya kitaifa na kimataifa.
HABARI NA MATUKIO
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala Akitoa Maelekezo kwa Maofisa, Askari na watumishi wa Uhamiaji katika Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JNIA) Jijini Dar es salaam.
Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Makao Makuu ya Uhamiaji |
MSHINDI WA SHINDANO BENKI YA NBC AKABIDHIWA PASIPOTI
Kamaishna Msaidizi wa uhamiaji na Mkuu wa kitengo cha pasipoti Dorah Luoga akikabidhi pasipoti kwa mshindi wa shindano la kuweka akiba katika Benki ya NBC Bi. Rebeka Joshua Marwa katika Ofisi ndogo ya Uhamiaji Makao Makuu Dar es salaam.
28 Desemba 2019
27 Desemba 2019
Uhamiaji yamlilia Ngonyani
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji
Dkt. Anna Peter Makakala jana tarehe 26 Disemba 2019 ameongoza waombolezaji
waliohudhuria ibada ya kumuaga Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu Sylvester
Peter Ngonyani aliyefariki usiku wa kuamkia tarehe 25 Disemba 2019.
Ibada hiyo ilifanyika nyumbani
kwa marehemu Toangoma Kigamboni, ambapo mbali na kuhudhuriwa na Kamishna
Jenerali, Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha, Maafisa Waandamizi wa
Uhamiaji, Maafisa, askari na watumishi wengine wa Uhamiaji walihudhuria katika ibada
hiyo.
Marehemu Sylvester Peter
Ngonyani aliajiriwa Idara ya Uhamiaji mwaka 1990
Marehemu
alizaliwa tarehe 09 Disemba 1964 katika Kijiji cha Ngoheranga
wilayani Malinyi Mkoa wa Morogoro, alisoma shule ya msingi Ngoheranga baadaye
Kibasila na Shycom kwa elimu ya sekondari. Pia elimu ya juu aliipata Chuo Kikuu
cha Mzumbe. Aliajiriwa na Idara ya Uhamiaji Mwaka 1990, na kushika nyadhifa
mbalimbali mpaka anastaafu mwishoni mwa mwaka huu marehemu Ngonyani alikuwa Mkuu
wa Kitengo cha Anuai za Jamii Makao Makuu ya Uhamiaji. Marehemu ameacha Watoto
watano na wajukuu wawili. Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina lake Lihimidiwe.
24 Desemba 2019
23 Desemba 2019
18 Desemba 2019
NAIBU WAZIRI MASAUNI AHITIMISHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHAMAJI DUNIANI
Naibu Waziri wa Mambo ya
Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni leo tarehe 18/12/2019 amehitimisha maadhimisho
ya Siku ya Kimataifa ya Wahamaji katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Uhamiaji
Kurasini Dar Es Salaam. Maadhimisho hayo ambayo yanafanyika kila mwaka
yanalenga kutambua haki za wahamaji pamoja na familia zao wanapokuwepo katika
nchi za kigeni.
Akihutubia katika Maadhimisho
hayo Mheshimiwa Masauni amempongeza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala
kwa kufanya mabadiliko makubwa kwenye Mifumo ya kutolea huduma zake kwa njia ya
Mtandao ambapo sasa mgeni anaweza kuomba Visa au Vibali vya Ukaazi, kufanya
malipo pamoja na kupokea kibali chake kwa njia ya mtandao akiwa mahali popote
Ulimwenguni bila ya kulazimika kufika katika Ofisi za Uhamiaji.
Aidha, Naibu Waziri aliongeza
kuwa Serikali imefanya marekebisho ya Sheria ya Uhamiaji kwa kuanzisha vibali maalumu
vya ukaazi kwa wahamiaji walowezi walioo hapa nchini ili kutatua tatizo la
uhamiaji haramu nchini. Pia Serikali imepunguza ada ya kibali cha Ukaazi kwa
wawekezaji wan je wenye asili ya Tanzania (Diaspora) kutoka Dola za Kimarekani
3050 hadi kufikia Dola 1000 ili kuhamasisha raia hao kuwekeza katika nchi yao
ya asili.
Awali akimkaribisha Naibu Waziri
Masauni, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala ameeleza kuwa kwa
sasa Idara ya Uhamiaji inaendelea kuzifanyia kazi changamoto zinazo wakabili
wateja wa huduma za Uhamiaji.
Dkt. Makakala aliongeza kuwa
kutokana na maboresho hayo, Waombaji wa huduma za Uhamiaji hususani Pasipoti hawatalazimika kuwasilisha katika
Ofisi za Uhamiaji Viambata vya nakala halisi watakapo hitaji Pasipoti. Badala yake
Viambato hivyo vitatakiwa kuwasilishwa kwa njia ya Mtandao pekee.
Katika Maadhimisho hayo Idara
ya Uhamiaji na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) wamesaini
Makubaliano ambayo yatawezesha mifumo ya huduma ya Taasisi hizo mbili kupeana
taarifa muhimu ikiwemo cheti cha kuzaliwa ambacho ni mojawapo ya kiambata
muhimu wakati wa kuomba Pasipoti.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)