Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

31 Desemba 2019

Heri ya Mwaka Mpya 2020


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Afanya Ziara ya Kushitukiza Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Nyerere. (JNIA)


Dar es salaam

Kamishina Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala leo amefanya ziara ya kushitukiza katika kituo cha Uhamiaji cha uwanja wa ndege wa Kimataifa wa  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JNIA) jijini Dar es salaam ikiwa ni lengo la kukagua utekelezaji wa Shughuli za uhamiaji katika kituo hicho.
Akifanya Kikao na Watumishi kituoni hapo Dkt.Makakala amewataka watumishi wote wanaofanya kazi katika kituo hicho kufanya kazi kwa nidhamu, utii, uhodari, na weledi  na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ikiwemo kutojihusisha na masuala ya rushwa.
Aidha ameapa kutowavumilia maafisa askari na watumishi wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na kwamba atawachukulia hatua kali za kinidhamu ikiwemo kuwafuta kazi na kuwafikisha mahakamani.
Sanjari na hilo amesisitiza pia kuongeza juhudi za ukusanyaji maduhuli ya serikali ili kuongeza pato la taifa na kuchochea maendeleo kwa faida ya kizazi cha sasa na baadae.
Ili kuongeza ufanisi zaidi katika utekelezaji wa majukumu ya ulinzi na usalama wa nchi kupitia mipaka na njia zote za kuingilia na kutokea  nchini, Dkt. Makakala amewataka maafisa na askari wote kushirikiana na vyombo vyote vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha nchi inakuwa salama.
Ziara ya Kamishina Jenerali ni muendelezo wa ziara za mara kwa mara katika kukagua shughuli za utendaji kazi ili kuhakikisha idara  inafikia malengo yake mahususi ya utendaji kwa  kutoa huduma za uhamiaji zenye kukudhi viwango vya kitaifa na kimataifa. 

HABARI NA MATUKIO

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala Akitoa Maelekezo kwa Maofisa, Askari na watumishi wa Uhamiaji katika Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere  (JNIA) Jijini Dar es salaam.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala Akitoa Maelekezo kwa Maofisa, Askari na watumishi wa Uhamiaji katika Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JNIA) Jijini Dar es salaam.

Baadhi ya Maofisa na Askari wa Uhamiaji Kituo cha Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es salaam wakimsikiliza kwa makini Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala (Hayupo Pichani) 
Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Makao Makuu ya Uhamiaji

MSHINDI WA SHINDANO BENKI YA NBC AKABIDHIWA PASIPOTI

Kamaishna Msaidizi wa uhamiaji na Mkuu wa kitengo cha pasipoti Dorah Luoga akikabidhi pasipoti kwa mshindi wa shindano la kuweka akiba katika Benki ya NBC Bi. Rebeka Joshua Marwa katika Ofisi ndogo ya Uhamiaji Makao Makuu Dar es salaam.

Makabidhiano hayo yalihudhuriwa na maafisa toka benki ya NBC  Pamoja na Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Mrakibu Mwandamizi Alhaj Ally Mtanda. Kwa ushindi huo Bi. Rebeka Joshua  Marwa anatarajia kwenda nchini Shelisheli.



27 Desemba 2019

Uhamiaji yamlilia Ngonyani

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala jana tarehe 26 Disemba 2019 ameongoza waombolezaji waliohudhuria ibada ya kumuaga Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu Sylvester Peter Ngonyani aliyefariki usiku wa kuamkia tarehe 25 Disemba 2019.

Ibada hiyo ilifanyika nyumbani kwa marehemu Toangoma Kigamboni, ambapo mbali na kuhudhuriwa na Kamishna Jenerali, Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha, Maafisa Waandamizi wa Uhamiaji, Maafisa, askari na watumishi wengine wa Uhamiaji walihudhuria katika ibada hiyo.

Marehemu Sylvester Peter Ngonyani aliajiriwa Idara ya Uhamiaji mwaka 1990

Marehemu alizaliwa  tarehe 09 Disemba 1964 katika Kijiji cha Ngoheranga wilayani Malinyi Mkoa wa Morogoro, alisoma shule ya msingi Ngoheranga baadaye Kibasila na Shycom kwa elimu ya sekondari. Pia elimu ya juu aliipata Chuo Kikuu cha Mzumbe. Aliajiriwa na Idara ya Uhamiaji Mwaka 1990, na kushika nyadhifa mbalimbali mpaka anastaafu mwishoni mwa mwaka huu marehemu Ngonyani alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Anuai za Jamii Makao Makuu ya Uhamiaji. Marehemu ameacha Watoto watano na wajukuu wawili. Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina lake Lihimidiwe.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akitoa heshima zake kwa Marehemu Sylvester Ngonyani 


Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha) Edward Chogero akitoa neno kwa niaba ya Uhamiaji


18 Desemba 2019

NAIBU WAZIRI MASAUNI AHITIMISHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHAMAJI DUNIANI










































Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni leo tarehe 18/12/2019 amehitimisha maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wahamaji katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Uhamiaji Kurasini Dar Es Salaam. Maadhimisho hayo ambayo yanafanyika kila mwaka yanalenga kutambua haki za wahamaji pamoja na familia zao wanapokuwepo katika nchi za kigeni.

Akihutubia katika Maadhimisho hayo Mheshimiwa Masauni amempongeza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala kwa kufanya mabadiliko makubwa kwenye Mifumo ya kutolea huduma zake kwa njia ya Mtandao ambapo sasa mgeni anaweza kuomba Visa au Vibali vya Ukaazi, kufanya malipo pamoja na kupokea kibali chake kwa njia ya mtandao akiwa mahali popote Ulimwenguni bila ya kulazimika kufika katika Ofisi za Uhamiaji.

Aidha, Naibu Waziri aliongeza kuwa Serikali imefanya marekebisho ya Sheria ya Uhamiaji kwa kuanzisha vibali maalumu vya ukaazi kwa wahamiaji walowezi walioo hapa nchini ili kutatua tatizo la uhamiaji haramu nchini. Pia Serikali imepunguza ada ya kibali cha Ukaazi kwa wawekezaji wan je wenye asili ya Tanzania (Diaspora) kutoka Dola za Kimarekani 3050 hadi kufikia Dola 1000 ili kuhamasisha raia hao kuwekeza katika nchi yao ya asili.

Awali akimkaribisha Naibu Waziri Masauni, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala ameeleza kuwa kwa sasa Idara ya Uhamiaji inaendelea kuzifanyia kazi changamoto zinazo wakabili wateja wa huduma za Uhamiaji.

Dkt. Makakala aliongeza kuwa kutokana na maboresho hayo, Waombaji wa huduma za Uhamiaji hususani  Pasipoti hawatalazimika kuwasilisha katika Ofisi za Uhamiaji Viambata vya nakala halisi watakapo hitaji Pasipoti. Badala yake Viambato hivyo vitatakiwa kuwasilishwa kwa njia ya Mtandao pekee.

Katika Maadhimisho hayo Idara ya Uhamiaji na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) wamesaini Makubaliano ambayo yatawezesha mifumo ya huduma ya Taasisi hizo mbili kupeana taarifa muhimu ikiwemo cheti cha kuzaliwa ambacho ni mojawapo ya kiambata muhimu wakati wa kuomba Pasipoti.