Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

22 Septemba 2020

CGI Dkt. Anna Makakala Akagua Maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Ofisi Mpya ya Makao Makuu ya Uhamiaji Tanzania.

Dodoma, Tanzania

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala mapema leo hii amekagua maendeleo ya Ujenzi wa Jengo Jipya la Ofisi za Uhamiaji Makao Makuu Dodoma.

Akiwa Katika Ukaguzi huo amejiridhisha na Ubora wa Ujenzi lakini ameitaka kampuni ya Ujenzi ya SUMAJKT Inayotekeleza Mradi huo Kuongeza Kasi ya Ujenzi ili kufikia malengo yaliyokusudiwa ya Kukamilisha kazi hiyo ya Ujenzi kwa Viwango vya Ubora wa Hali ya Juu na kwa  wakati muafaka uliopangwa.

Ujenzi huo ni matokeo chanya ya Serikali ya awamu ya tano Kuhamishia Makao Makuu ya Nchi rasmi Jijini Dodoma   Chini ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Aidha Mhe. Rais Dkt. Magufuli wakati wa Uzinduzi wa Mfumo wa Uhamiaji  Mtandao (e-Immigration) uliofanyika Jijini Dar e salaam Tarehe 31 Januari 2018 alitoa Tsh.Bilioni 10 kwa ajili ya Kuanza Ujenzi huo wa Ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji Tanzania ambao utakamilika hivi karibuni ukiwa na ghorofa nane.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala  Akitoa Maelekezo kwa Wataalamu wa Ujenzi wa Kampuni ya SUMAJKT Mapema leo hii Jijini Dodoma Ili kuongeza Kasi ya Ujenzi wa Jengo la Ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji Tanzania


  Mtaalamu wa Ujenzi Kutoka Kampuni ya Ujenzi ya SUMAJKT Akitoa maelezo ya awali ya maendeleo ya Ujenzi kwa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala  


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala  akitoa maelekezo



Ujenzi Unaendelea  




Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala  akitoa maelekezo



Ujenzi Unaendelea
Mafundi Wakiendelea na Kazi
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala  akiendelea na Ukaguzi





Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala  akiendelea na Ukaguzi wa Ujenzi




Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala  akishuka katika Ngazi mara baada ya Kumaliza Ukaguzi na Kutoa Maelekezo ya Kuhakikisha Kasi inaongezeka ya Ujenzi



Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala   akisisitiza jambo kwa Wataalamu wa Ujenzi wa SUMAJKT


Ujenzi ukiendelea  

Mtaalamu wa Ujenzi kutoka SUMAJKT akimhakikishia Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala Kuongeza Kasi ya Ujenzi 




Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania Dkt. Anna Makakala  Akisaini Kitabu cha Wageni baada ya kumaliza Ukaguzi wa Maendeleo ya Ujenzi wa Ofisi Mpya za Uhamiaji Makao Makuu Dodoma (Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)