Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

28 Februari 2020

KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI AKAGUA UJENZI WA NYUMBA ZA WATUMISHI NA JENGO LA MAKAO MAKUU DODOMA

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala amefanya ziara ya kutembelea eneo la  Ujenzi wa Mradi wa Nyumba wa Iyumbu Satellite Centre pamoja na NCC panapojengwa Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dodoma leo tarehe 28 Februari 2020.

Idara ya Uhamiaji itegemea kupokea nyumba mpya 40 ikiwa ni sehemu ya pili ya jumla ya nyumba 103 zilizotolewa  na Rais wa awamu ya Tano Mhe. John Joseph Pombe Magufuli kwa ajili ya makazi ya Maafisa, askari na watumishi raia wa Idara hiyo  mwaka 2017.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala akisikiliza maelezo ya maendeleo ya umaliziaji ujenzi wa nyumba 40  za Idara hiyo toka kwa Mkurugenzi wa Mauzo, Shirika la Nyumba la Taifa, Ndg. Itandula Gambaladi leo asubuhi, eneo la Iyumbu, jijini Dodoma.


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala akisaini Kitabu cha wageni baada ya kuwasili eneo la Karakana ya Ujenzi wa Mradi wa Nyumba wa Iyumbu Satellite Centre jijini Dodoma leo, Idara ya Uhamiaji itegemea kupokea nyumba mpya 40 ikiwa ni sehemu ya pili ya jumla ya nyumba 103 zilizotolewa  na Rais wa awamu ya Tano Mhe. John Joseph Pombe Magufuli kwa ajili ya makazi ya Maafisa, askari na watumishi raia wa Idara hiyo  mwaka 2017.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala akikagua Maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji leo asubuhi eneo la NCC, jijini Dodoma.




#Ijumaa Njema


24 Februari 2020

Waziri Simbachawene Atoa Maagizo haya kwa Jeshi la Uhamiaji Tanzania.

Dar es salaam, Tanzania
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi Mhe. George Simbachawene aliyeteuliwa hivi karibuni na Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya ziara ya Kujitambulisha katika Jeshi la Uhamiaji Tanzania na kufanya mazungumzo na Viongozi Waandamizi wa Jeshi hilo Katika Ofisi ndogo ya Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam.

Akitoa Maelekezo na Mpango Mkakati wake katika Wizara amelipongeza Jeshi la Uhamiaji kwa kufanya kazi kwa ufanisi na weledi wa hali ya juu.

“Niwe Mkweli tu, Kusema kweli hata viongozi wakubwa wanaridhishwa sana na utendaji kazi wenu, Mhe. Rais anaridhishwa sana na kazi yenu mnayofanya endeleeni kufanya kazi kwa uhodari,ufanisi na kwa weledi wa hali ya juu kwa manufaa  ya sasa na kizazi kijacho” Alisema Mhe. Waziri Simbachawene.

Mhe. Waziri aliongeza Kwamba tofauti ya Jeshi la Uhamiaji na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ni kwamba ninyi ni  ni Jeshi lakini linaloshughulika sana na mambo ya kidiplomasia (Diplomatic Army)  mchakato mnaofanya ni wa kushughulika na wageni wanaokuja kwa madhumuni tofauti tofauti wakiwemo wawekezaji, watalii na kuhakikisha wanaingia na kutoka salama.

“Mnashughulika na maeneo nyeti sana, kwenye hili kusema kweli tunafurahi kwa namna mlivyojipanga na mnafanya kazi vizuri hongereni sana, hata katika Maelekezo yangu ninapokutana na viongozi sioni wa kuwanyoshea vidole endeleeni kuchapa kazi” Alisema

Aidha amesisitiza kuendelea kudhibiti na kusimamia kwa makini Uingiaji na utokaji wa raia wa Tanzania na wageni ikiwemo kudhibiti uingiaji wa wahamiaji haramu na kupambana na Biashara haramu ya binadamu (Human Trafficking & Smuggling) katika mipaka yote.

Akitoa taarifa ya utendaji kazi ya Jeshi la Uhamiaji kwa Mhe. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Gerald Kihinga alieleza kwamba moja ya jukumu kubwa la Jeshi hilo ni kulinda usalama wa nchi na mipaka yake kwa kudhibiti uingiaji ukaaji na utokaji nje kwa raia na wageni kwa mujibu wa sheria,  kanuni na taratibu zilizopo.

Aidha Kaimu Kamishna Jenerali Kihinga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Kuajiri askari wapya 400 waliomaliza mafunzo yao ya kujitolea katika Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakiwa na Utii, Uhodari na weledi wa hali ya juu katika kulitumikia Taifa lao na sasa wanatekeleza majukumu yao ipasavyo ndio maana unaona idadi kubwa ya kukamata wahamiaji haramu imeongezeka sana kwa muda mchache yaani hakuna atakayepona kwa sasa kwani tuko imara zaidi.

Mbali na hilo amewatahadharisha wasafirishaji wa wahamiaji haramu na wale wanaohusika na biashara ya binadamu (Human Trafficking & Human Smuggling) kuacha mara moja shughuli hizo kwani wakikamatwa watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kutaifisha chombo kilichohusika kubeba wahamiaji haramu, nyumba iliyowahifadhi, lakini pia kifungo cha kwenda jela miaka 20, au faini milioni 20 au vyote kwa pamoja hivyo waache mara moja kwani watashughulikiwa ipasavyo.

Ikumbukwe kuwa ziara hii ni ya kwanza kwa Mhe. Waziri George Simbachawene Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi toka kuteuliwa kwake hivi karibuni na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ambapo amekutana na viongozi waandamizi wa Jeshi la Uhamiaji Tanzania ikiwa ni moja ya taasisi ya vyombo vya ulinzi na usalama nchini iliyopo chini ya wizara hiyo na Kutoa Maelekezo muhimu ya kusonga mbele.
  
HABARI PICHA NA MATUKIO
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene akiwasili katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam alipofanya ziara ya kikazi na kukutana na Viongozi waandamiizi wa Uhamiaji

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene (Kushoto) akisasilimiana na Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Gerald Kihinga  katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene (Kushoto) akisasilimiana na Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Vibali vya Ukaazi, Visa na Pasi Mary Palmer (ndc) katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam 


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene (Kushoto) akisasilimiana na Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka Samwel Mahirane katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene (Kushoto) akisasilimiana na Mkuu wa Kitengo cha Uratibu na Utawala Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji  Sophia Gunda katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene (Kushoto) akisasilimiana Msemaji Mkuu wa Jeshi la Uhamiaji Mrakibu Mwandamizi Alhaj Ally Mtanda katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam 





Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene akipokea maelezo katika chumba cha kuchukulia alama za vidole ikiwa ni sehemeu moja wapo ya hatua za kuchakatwa kwa pasipoti mpya ya Kieleketroniki.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene (Kushoto) akipokea maelezo katika chumba cha kuchakata pasipoti na kuzikagua ubora unaokidhi viwango vya Kimataifa  

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene akifurahia aina tofautu tofauti za pasipoti ya Kielektroniki katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam 


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene (Kushoto) akimsikiliza kwa makini Kamishna wa Uhamiaji anayesimamia Divisheni ya Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka Samwel Mahirane katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi  Mhe. George Simbachawene (Kulia) akipokea maelezo ya namna Divisheni yake  katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam 


Baadhi ya Viongozi waandamizi wa Jeshi la Uhamiaji wakimsikiliza kwa makini waziri Simbachawene








Picha ya Pamoja




Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Simbachawene akizungumza na waandishi wa Habari



(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano  Uhamiaji Makao Makuu)

14 Februari 2020

Chuo cha Ulinzi wa Taifa NDC Wafanya Ziara ya Mafunzo katika Idara ya Uhamiaji Tanzania

Dar es salaam, Tanzania
Idara ya Uhamiaji Tanzania leo imepokea ugeni kutoka chuo cha Ulinzi wa Taifa NDC kwa ajili ya ziara ya  kupatiwa mafunzo ya namna Idara ya Uhamiaji inavyofanya shughuli zake katika ulinzi wa Taifa na Maendeleo ya Kiuchumi.

Ziara hiyo ya mafunzo imefanyika katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar e salaam ikiongozwa na Brigedia Jenerali Msola na kupokelewa na  Kamishna wa Uhamiaji Divisheni ya Uraia na Pasipoti Gerald Kihinga ambae alimwakilisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala.

Katika mafunzo hayo, mada mbalimbali ziliweza kuwasilishwa na Maafisa kutoka Idara ya uhamiaji hususani Pasipoti, Visa za Kielektroniki, Uraia pamoja na Mifumo inayotumika katika utoaji wa Pasipoti na visa za kieletroniki.


Aidha, Washiriki wa ziara hiyo walipata fursa ya kuuliza maswali na kujibiwa ipasavyo sanjari na kutembelea na kujionea namna mifumo mbalimbali ya Uhamiaji inavyofanya kazi na kuonyesha kufurahishwa na jinsi mifumo hiyo inavyorahisisha utoaji wa huduma za uhamiaji kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa.

Kwa upande wao washiriki walimpongeza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji kwa mafunzo waliyoyapata na kuongeza kuwa, mafunzo hayo yatawajengea uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi na weledi mkubwa hususani katika kuwahudumia Watanzania, Afrika na Dunia kwa Ujumla.

HABARI NA MATUKIO KATIKA MPICHA
Brigedia Jenerali Chelestino Msola (Kushoto) akimkabidhi zawadi kutoka NDC Kamishna wa Uhamiaji Divisheni ya Pasipoti na Uraia Gerald Kihinga anayemwakilisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania
Brigedia Jenerali Chelestino Msola (Kushoto) akimkabidhi zawadi kutoka NDC Kamishna wa Uhamiaji Divisheni ya Pasipoti na Uraia Gerald Kihinga anayemwakilisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Tanzania



Brigedia Jenerali Chelestino Msola Mkuu wa Msafara kutoka NDC akisaini kitabu cha Wageni Katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Dar es salam.
Washiriki wa Mafunzo kutoka NDC wakipewa maelezo mbalimbali kuhusu Huduma zitolewazo na Idara ya Uhamiaji hususani katika Mfumo wa Kidijitali wa Uhamiaji Mtandao walipotembelea moja ya eneo la kutolea huduma hizo




Washiriki kutoka NDC Wakifuatilia kwa makini Mafunzo wanayopewa na Maofisa wa Uhamiaji Tanzania
Kamishna wa Vibali vya Ukaazi na Pasi Mary Palmer Akitolea ufafanuzi kuhusu baadhi ya hoja zilizoulizwa na washiriki kutoka NDC




Baadhi ya washiriki kutoka NDC ambao pia ni kutoka Mataifa mbalimbali wakijitambulisha
Mrakibu wa Uhamiaji Eliud Ikomba akitoa Utangulizi wa Mada iliyotolewa katika Mafunzo ya washiriki kutoka NDC


Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji Azizi Kirondomara Kutoka Kitengo cha Uhusiano Makao Makuu akitoa Mada kwa Washiriki wa Mafunzo kutoka NDC


Baadhi ya Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi NDC wakifuatilia kwa makini mafunzo wanayopewa kuhusa huduma za Idara ya Uhamaiaji Tanzania


Mmoja wa Washiriki Kutoka NDC Akiuliza swali baada ya kupewa mafunzo ya Uhamiaji
Picha ya Pamoja Washiriki wa Mafunzo kutoka NDC Wakiwa na Maofisa wa Uhamiaji  Katikati ni Kamishna wa Pasipoti na Uraia Gerald Kihinga (Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Makao Makuu)