Visitors
31 Januari 2018
Fahamu kuhusu Uhamiaji Mtandao
Uhamiaji Mtandao (e-immigration) ni muunganiko
wa mifumo mbalimbali ambayo imesanifiwa kufanya kazi kwa pamoja na kutoa
taarifa kwa watumiaji na wadau wa huduma za kiuhamiaji.
Kupitia teknolojia hiyo, Idara itaweza kutoa;
Kupitia teknolojia hiyo, Idara itaweza kutoa;
·
Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki (e-
Residence Permit),
·
Pasipoti za Kielektroniki (e-Passport)
·
Pamoja na kusimamia masuala ya mipaka
kielektroniki (e-Border Management).
· Viza za kielektroniki (e-Visa)
Mfumo huo wa Uhamiaji Mtandao unalenga kutusaidia;
· Viza za kielektroniki (e-Visa)
Mfumo huo wa Uhamiaji Mtandao unalenga kutusaidia;
· kutoa Pasipoti ya
Kielektroniki ya Afrika Mashariki (e-Passport) ambayo imetengenezwa kwa kutumia
teknolojia ya kisasa ambapo itakuwa na ‘chip’ iliyobeba
taarifa mbalimbali za mwombaji pamoja na alama nyingi za kiusalama “Security
Features”
· Mfumo utasaidia
kudhibiti na kuwezesha Uingiaji, Ukaaji na Utokaji wa Raia na Wageni wanaoingia
nchini kwa madhumuni mbalimbali hususan katika maeneo ya mipakani ikiwa ni pamoja
na kutunza kumbukumbu zao. Hii itasaidia kuzuia ongezeko la wahamiaji haramu
nchini.
· Pia utasaidia usimamizi
wa utoaji viza na mwombaji atawasilisha maombi yake kwa njia ya kielektroniki;
hii itasaidia kupata taarifa za malipo ya viza kwa wakati na, kudhibiti upotevu
wa maduhuli ya Serikali.
26 Januari 2018
Mkutano wa Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na waandishi wa Habari Makao Makuu ya Uhamiaji
Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi jana tarehe 25 Januari 2018 alifanya mkutano na waandishi wa habari katika Ofisi za Uhamiaji Makao Makuu.
Katika mkutano huo, alitoa maagizo mbalimbali na pia kusimamisha utoaji wa pasipoti kwa vijana wanaokwenda nje ya nchi kufanya kazi za ndani na nyinginezo ambapo imeripotiwa kuwa pindi wakiwa huko ughaibuni huteswa, kunyanyaswa na hata kuuwawa.
Katika mkutano huo, alitoa maagizo mbalimbali na pia kusimamisha utoaji wa pasipoti kwa vijana wanaokwenda nje ya nchi kufanya kazi za ndani na nyinginezo ambapo imeripotiwa kuwa pindi wakiwa huko ughaibuni huteswa, kunyanyaswa na hata kuuwawa.
25 Januari 2018
UHAMIAJI YAKABIDHIWA RASMI NYUMBA ZA IYUMBU DODOMA
Idara ya Uhamiaji imekabidhiwa nyumba 63 ambazo zilizinduliwa na
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Joseph Magufuli
mwishoni mwa mwaka jana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
Nyumba hizo ambazo zipo katika
eneo la Iyumbu Manispaa ya Dodoma zilipokelewa na Kamishna Uhamiaji (Utawala na
Fedha) Peter Chogero kutoka kwa Maafisa wa Shirika la Nyumba jana Jumatano 25 Januari 2018.
"Nashukuru sana
kukabidhiwa hizi nyumba kwa kuwa sasa maafisa wataweza kuhamia mara moja. Idara
inatoa shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais kwa kutupatia nyumba hizi"
Alisema Kamishna Chogero.
21 Januari 2018
Huduma halali za Pasipoti, Epuka Upotoshwaji.
• Pasipoti
hutolewa kwa Raia wa Tanzania tu.
• Na ni haki
ya kila Mtanzania, Timiza wajibu wako.
• Zingatia
Taratibu za Uombaji na Utoaji wa Pasipoti.
Maombi ya Pasipoti huwasilishwa na mwombaji mwenyewe katika Ofisi za
Uhamiaji Makao Makuu, Afisi ya Uhamiaji Zanzibar, au kwenye ofisi yoyote ya
Uhamiaji Mkoa ama Wilaya anayoishi mwombaji au Ofisi za Balozi za Tanzania kwa waombaji
wanaoishi nchi za nje.
Huduma zote za Uhamiaji hazina Uwakala – Epuka Mawakala/Vishoka
17 Januari 2018
NAMNA YA KUJAZA FOMU MTANDAONI
NAMNA YA KUJAZA FOMU ZA
MAOMBI YA PASIPOTI
KWA NJIA YA MTANDAO.
2. NENDA KATIKA KITUFE
KILICHOANDIKWA
e - Services. (https://www.immigration.go.tz/ppt_application/)
3. NENDA KWENYE PASSPORT APPLICATION FORM (BOFYA).
4. (i)KWA
MTU AMBAYE ANAJAZA FOMU KWA MARA YA KWANZA KWA NJIA YA MTANDAO ANATAKIWA
KUBOFYA NAMBA 1. OMBI JIPYA.
(ii) KWA AMBAYE
ALIKWISHAJAZA FOMU MTANDAONI HAPO KABLA, NA KUPEWA NAMBA YA OMBI HUSIKA,
ATACHAGUA OMBI LINALOENDELEA ATAINGIZA NAMBA YAKE YA OMBI NA JINA LAKE LA
UKOO.
5. KWA
MTU ANAYEJAZA KWA MARA YA KWANZA ATALETEWA MWONGOZO WENYE MAELEZO YA SIFA ZA
MWOMBAJI. BAADA YA KUSOMA MAELEZO YA UKURASA HUU. BOFYA KITUFE CHA KUKUBALIANA NA MAELEZO YALIYOPO KWENYE UKURASA HUU NA
KISHA UTAENDELEA.
6. BAADA
YA KUKAMILISHA HATUA YA TANO, MWOMBAJI ATAPELEKWA KATIKA UKURASA WA ONLINE PASSPORT APPLICATION NA HAPO ATATAKIWA
KUJAZA KILA KIPENGELE KUANZIA SEHEMU YA TAARIFA
BINFSI.
7. UNAPOJAZA
ZINGATIA KUFUATA MAELEKEZO YA NAMNA YA UJAZAJI (FORMAT) YALIYO AINISHWA KWENYE UKURASA HUSIKA.
8. BAADA
YA KUKAMILISHA BOFYA KITUFE - KUPAKUA
FOMU.
9. ITAKULETEA
FOMU YAKO YA MAOMBI ULIYOJAZA NA HATI YA DHAMANA. UTAHAKIKI TAARIFA ZAKO NA
KISHA KUICHAPA (PRINT) FOMU HIYO PAMOJA NA HATI YA DHAMANA HUSIKA.
10. HATI YA DHAMANA INATAKIWA
IJAZWE NA WATU WATANO (05) TOFAUTI, YAANI WADHAMINI WAWILI (02) NA MASHAHIDI
WATATU (03).
NB:
FOMU YA MAOMBI YA PASIPOTI INAWEZA KUJAZWA MAHALI POPOTE
PENYE HUDUMA YA INTERNET, AMBAPO MWOMBAJI ALIPO, NA WALA MWOMBAJI HALAZIMIKI
KWENDA KUJAZIA FOMU HIYO JIRANI NA OFISI ZA UHAMIAJI.
Imetolewa na Kitengo cha Mahusiano-Uhamiaji Makao Makuu
Ukaguzi wa Wageni nchini Mkoa wa Kagera
Sheria Ya Uhamiaji Sura 54 Rejeo la 2016 inampa mamlaka Afisa Uhamiaji kumsimamisha mtu yeyote na kumhoji juu ya Uhalali wake wa kuwepo nchini Tanzania. Hapa ni Afisa Uhamiaji kutoka Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kagera Sajini Elia Mlay akimkagua raia wa Poland kujiridhisha uhalali wake wa kuishi nchini.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)