Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

31 Januari 2018

Fahamu kuhusu Uhamiaji Mtandao

Uhamiaji Mtandao (e-immigration) ni muunganiko wa mifumo mbalimbali ambayo imesanifiwa kufanya kazi kwa pamoja na kutoa taarifa kwa watumiaji na wadau wa huduma za kiuhamiaji.

Kupitia teknolojia hiyo, Idara itaweza kutoa;
·           Vibali vya Ukaazi vya Kielektroniki (e- Residence Permit),
·           Pasipoti za Kielektroniki (e-Passport)
·           Pamoja na kusimamia masuala ya mipaka kielektroniki (e-Border Management).
·           Viza za kielektroniki (e-Visa)

Mfumo huo wa Uhamiaji Mtandao unalenga kutusaidia;
·         kutoa Pasipoti ya Kielektroniki ya Afrika Mashariki (e-Passport) ambayo imetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa ambapo itakuwa na chip’ iliyobeba taarifa mbalimbali za mwombaji pamoja na alama  nyingi za kiusalama “Security Features”
·         Mfumo utasaidia kudhibiti na kuwezesha Uingiaji, Ukaaji na Utokaji wa Raia na Wageni wanaoingia nchini kwa madhumuni mbalimbali hususan katika maeneo ya mipakani ikiwa ni pamoja na kutunza kumbukumbu zao. Hii itasaidia kuzuia ongezeko la wahamiaji haramu nchini.

·         Pia utasaidia usimamizi wa utoaji viza na mwombaji atawasilisha maombi yake kwa njia ya kielektroniki; hii itasaidia kupata taarifa za malipo ya viza kwa wakati na, kudhibiti upotevu wa maduhuli ya Serikali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni