Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

25 Januari 2018

UHAMIAJI YAKABIDHIWA RASMI NYUMBA ZA IYUMBU DODOMA

Idara ya Uhamiaji imekabidhiwa nyumba 63 ambazo zilizinduliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Joseph Magufuli mwishoni mwa mwaka jana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Nyumba hizo ambazo zipo katika eneo la Iyumbu Manispaa ya Dodoma zilipokelewa na Kamishna Uhamiaji (Utawala na Fedha) Peter Chogero kutoka kwa Maafisa wa Shirika la Nyumba jana Jumatano 25 Januari 2018.

"Nashukuru sana kukabidhiwa hizi nyumba kwa kuwa sasa maafisa wataweza kuhamia mara moja. Idara inatoa shukrani nyingi kwa Mheshimiwa Rais kwa kutupatia nyumba hizi" Alisema Kamishna Chogero.










Hakuna maoni:

Chapisha Maoni