Visitors
25 Juni 2021
KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI, DKT. A.P. MAKAKALA, AFUNGUA WARSHA KUHUSU USALAMA WA MIPAKA KWA NJIA YA MTANDAO
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji DKT. A. P. Makakala mapema wiki hii afungua warsha kuhusu Usalama wa Mipaka, warsha hiyo inayoendeshwa katika Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Moshi, ilifunguliwa na Kamishna Jenerali kwa njia ya mtandao akiwa Zanzibar.
Katika hotuba yake Dkt. Makakala alifahamisha kuwa usalama wa mipaka lazima upewe kipaumbele hasa kwa kuzingatia maendeleo ya sayansi na teknolojia ambayo yanachangia uhalifu unaovuka mipaka (Transnational Organized Crimes) duniani kote.
Dkt. Makakala aliwataka washiriki wa warsha hiyo kuwa makini na kuzingatia mafunzo watakayopatiwa ili waweze kuwafundisha wenzao ambao hawakupata fursa ya kushiriki mafunzo hayo pamoja na kuwataka kutumia mbinu mpya walizofundishwa katika marsha hiyo katika kudhibiti Uhalifu unaovuka mipaka.
Maafisa 32 walioshiriki katika warsha hiyo kutoka vituo mbali mbali vya kuingilia na kutokea watu nchini kutoka Tanzania Bara na Zanzibar walijifunza ukaguzi wa nyaraka, mienendo na mabadiliko ya mbinu za kudhibiti ugaidi, dawa za kulevya, umuhimu wa intelijensia katika kusimamia ulinzi na usalama wa mipaka pamoja na matumizi ya mifumo mbalimbali ya Uhamiaji.
MATUKIO KATIKA PICHA: ZIARA YA NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI UHAMIAJI
Dkt. Anna Makakala akisoma taarifa ya Utendaji kazi wa Idara ya Uhamiaji mbele ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Khamis Hamza Khamis |
Baadhi ya Maafisa, Askari na watumishi wa Idara ya Uhamiaji wakimsikiliza Mhe. Khamis wakati akiongea nao nje ya jengo ya ofisi za Makao Makuu ya Uhamiaji Dodoma |
Naibu Waziri Mhe. Khamis Hamza Khamis akiandika katika kumbukumbu zake wakati akiskiliza taarifa kutoka kwa Dkt. Makakala |
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Khamis Hamza Khamis akiongea na Maafisa, Askari na Watumishi wa Idara ya Uhamiaji Dodoma |
Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha) Hamza Ismail Shaabani akitoa taarifa ya maendeleo wa jengo la Uhamiaji Makao Makuu jijini Dodoma |
11 Juni 2021
KAMISHNA WA UHAMIAJI ZANZIBAR AWATAKA WANANCHI KUFICHUA WAHAMIAJI WASIOFUATA SHERIA
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari Masoud Sururu mapema wiki hii atembelea vipenyo mbali mbali katika Mkoa wa Kusini na Kaskazini Pemba ili kujionea mazingira halisi pamoja na kutoa elimu kwa Wananchi juu ya umuhimu wakushirikiana na Idara ya Uhamiaji katika kutoa taarifa kwa Wahamiaji wasiofuata sheria za Uhamiaji.
Akizungumza
na Wananchi wanaoishi pembezoni mwa vipenyo vya mto wa kuwa na Mkia wa ng’ombe huko
Kaskazini Pemba aliwataka wananchi kushiriki katika kuimarisha ulinzi kwenye vipenyo
kwa kutoa taarifa kwa Idara ya Uhamiaji kuhusu chombo chochote kinachokusudia
au kuonekana katika eneo hilo ili taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa.
Kamishna
Sururu aliwafahamisha Wananchi hao athari za Uhamiaji haramu ikiwa ni pamoja na
kuhatarisha usalama wa nchi na Serikali kukosa mapato yatokanayo na malipo ya
visa.
Aidha
Wananchi walitaka kupatiwa elimu zaidi ya Uhamiaji ili wawe na uwezo wa kuwabaini
Wahamiaji Haramu katika maeneo yao. Wananchi hao waliahidi kutoa mashirikiano
na Idara ya Uhamiaji.
Nae Sheha
wa Shehia ya Gando Maalim Karim Mangunja alibainisha kuwa hakuna vyombo vya kigeni
vinavyoingia katika vipenyo hivyo hata hivyo aliahidi pale ikitokea chombo
chochote ikitakachotiliwa shaka ataijuilisha Idara ya Uhamiaji.