Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

09 Februari 2021

KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI AFANYA ZIARA YA KIKAZI JIJINI DAR ES SALAAM

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala mnamo siku ya Jumatatu Februari 8, 2020 amefanya ziara ya kikazi ya siku moja jijini Dar es salaam. Katika ziara hiyo, Dkt. Makakala amemtembelea Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Aboubakar Kunenge na kuongea nae kuhusu masuala ya uhamiaji katika mkoa huo.

Kamishna Jenerali pia alitembelea ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Ubungo na kuongea na Mkuu wa Wilaya Mh. Kisare Makori, ambapo pia alifanya ukaguzi wa ofisi ya Uhamiaji (W) Ubungo na kuzungumza na Askari pamoja na Watumishi kwa lengo la kutatua changamoto zinazowakabili. Baada ya mazungumzo hayo, Kamishna Jenerali alikwenda kukagua kituo kipya cha Uhamiaji ndani ya stendi mpya ya Mabasi Ubungo.

Ziara hiyo ya Siku moja jijini Dar es salaam ilifikia tamati kwa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji  kukagua kiwanda cha uchapishaji na ushonaji cha Idara ya uhamiaji kilichopo kijichi Jijini Dar es salaam. Katika ukaguzi huu alisisitiza watendaji waongeze kasi na weledi ili kufikia malengo yanayotarajiwa.


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akisikiliza maelezo ya namna ya shughuli za ushonaji zinavyofanyika katika Kiwanda cha Ushonaji cha Uhamiaji, Kijichi Dar es salaam



Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Abubakar Kunenge mara baada ya mazungumzo ya kikazi katika ofisi za mkuu huyo wa mkoa.









Hakuna maoni:

Chapisha Maoni