Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

14 Mei 2019

IDARA YA UHAMIAJI YAIKABIDHI SUMAJKT MRADI WA UJENZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU DODOMA

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna P. Makakala jana alikabidhi  Mradi wa Ujenzi wa jengo la ghorofa nane ambalo litakuwa Makao Makuu mpya ya Uhamiaji  eneo la NCC, Kitalu na 18 na 19, jijini Dodoma  kwa wakandarasi wa SUMAJKT.
Kamishna Jenerali alisema " tunaijua sifa ya SUMAJKT kupitia mifano mbalimbali ya  majengo bora ambayo wameyakamilisha kwa wakati, na kwa ukweli huu nina imani kubwa nao ya kwamba jengo letu litajengwa kwa ustadi wa hali ya juu na hivyo kuwa ni moja ya majengo ya kisasa yanayovutia hapa jijini Dodoma"
 Kwa upande mwingine tukio hili lilihudhuliwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Martin Busungu na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT, Kanali Mabele ambaye aliahidi kuwa shirika lake litajenga jengo ambalo litakuwa ni kioo cha ubora wa kazi zao na kwamba watu hawata hitaji kwenda jijini Dar es Salaam kuona mifano ya kazi zao bali hapa Dodoma tu.
Aidha, tukio  hili  lilishuhudiwaa na Mkuu wa Timu ya washauri waelekezi wa Mradi, Dkt. Msanifu Majenzi, Isabela Mtani kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi, Dar es Salaam  ambaye alisema kuwa makabidhiano ya Mradi huo wa Ujenzi kati ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni mmiliki na SUMAJKT ambayo ni Mkandarasi yatafuatiwa na shughuli nyingi ambazo zimepangwa kwenda kwa haraka sana na bila kuathili ubora wa kazi yenyewe na jengo linalojengwa.
Mradi wa jengo hilo ambalo litakuwa kubwa kuliko lile la Kurasini, Dar es Salaam na ambalo lilikuwa Makao Makuu ya zamani linatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miezi 18, na kuiwezesha Idara ya Uhamiaji kuanza kutumia jengo bora lenye hadhi ya kimataifa jijini Dodoma. 
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna P. Makakala (katikati) na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Martin Busungu (kulia) kwa pamoja wakisikiliza maelezo ya vipengele vya utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji eneo la NCC, Kitalu na 18 na 19, jijini Dodoma toka kwa Mshauri Mwelekezi wa Mradi, Dkt. Msanifu Majenzi, Isabela Mtani wa Chuo Kikuu cha Ardhi , Dar es Salaam (kushoto ) wakati wa tukio la makabidhiano ya Mradi huo wa Ujenzi kati ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni mmiliki na SUMAJKT ambayo ni Mkandarasi. Walioketi mbele, kulia ni Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha), Kamishna Peter Chogero na kushota ni Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT, Kanali Mabele. 

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna P. Makakala (katikati) akisisitiza jambo kwa timu za Mshauri Mwelekezi na Wajenzi wa Mradi wa Ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji eneo la NCC, Kitalu na 18 na 19, jijini Dodoma. Walioketi, kulia  ni Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Martin Busungu na kushoto kwake ni Mkuu wa Timu ya washauri waelekezi wa Mradi, Dkt. Msanifu Majenzi, Isabela Mtani kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi, Dar es Salaam wakati wa makabidhiano ya Mradi huo wa Ujenzi kati ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni mmiliki na SUMAJKT ambayo ni Mkandarasi.  

09 Mei 2019

Epuka Msongamano, Wahi sasa! #ePassport


UHAMIAJI YATOA ONYO KALI KWA MAWAKALA (VISHOKA) WANAOTUMIA VIBANDA VYA WAJASIRIAMALI VILIVYOPO MKABALA NA OFISI YA UHAMIAJI MAKAO MAKUU KUWATAPELI WANANCHI.

Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Hanelore Manyanga amekutana na wafanya biashara na wajasiriamali wanaofanya biashara katika mtaa wa Loliondo, Kurasini - Jijini Dar es salaam. Mtaa huo upo Mkabala na Ofisi za Uhamiaji Makao Makuu na kuna shughuli mbalimbali za biashara ikiwamo Mamalishe, Mawakili, Wapiga picha (Passport size) pamoja na watoa huduma za Stationaries.

Kamishna Manyanga amewataka wafanya biashara hao kuisaidia Idara ya Uhamiaji kupiga vita mawakala wa huduma za Uhamiaji (Vishoka ambao wanawatapeli wananchi wanaohitaji huduma za Uhamiaji katika maeneo hayo.

“Kumekuwepo na wimbi la Matapeli wanaojifanya kuwa Maafisa Uhamiaji wanawatapeli Wananchi kwa kuchukua pesa zao na kuwaahidi kuwasaidia kupata huduma za Uhamiaji ikiwa ni pamoja na Pasipoti, Viza, na Hati za Ukaazi kwa haraka. Kupitia kikao hiki nawaagiza kuwa mfanye biashara kwa mujibu wa matakwa ya leseni zenu kama inatokea kuna mtu ambaye siyo mhusika au anatumia vibanda vyenu kuwatapeli wananchi, tafadhali toeni taarifa Uhamiaji” alisema Kamishna Hanelore Manyanga

Aidha, Kamishna Manyanga aliongeza kuwa Idara ya Uhamiaji imedhamiria kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wale wote wanaojifanya Maafisa Uhamiaji na kuwatapeli Wananchi.
Wakitoa maoni yao katika kikao hicho baadhi ya wajasiriamali hao wametoa maoni yao na kuonesha kuchukizwa na vitendo hivyo ambavyo vinafanywa na watu ambao siyo waadilifu na kuchafua taswira nzuri ya Idara ya Uhamiaji na biashara zao kwa ujumla.

“Ni jambo jema kualikwa hapa kujadili suala hili, hata sisi tumekuwa tukichukizwa na hawa watu lakini tunashindwa kutoa taarifa kwani hatujui tumwambie nani, unakuta mtu anakuja pale mgahawani na mtu wanasaidiana kujaza fomu za Uhamiaji na baadae wanaondoka. Kupitia kikao hiki sasa tutakuwa tunatoa taarifa Uhamiaji lakini tunaomba tukitoa taarifa hizo zifanyiwe kazi na pia taarifa hizo ziwe siri” alisema Bi. Praise

Kupitia Kikao hicho wafanya biashara hao kwa pamoja wameahidi kushirikiana na Idara ya Uhamiaji na kuwafichua Mawakala/Vishoka wanaotumia Ofisi za mawakili, stationeries na migahawa kufanyia shughuli za Uhamiaji ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa yeyote atakayejihushisha na kazi za Uhamiaji katika maeneo yao ikiwa ni pamoja kufikishwa Mahakamani.

Kwa upande wake Kamishna wa Uhamiaji, Uraia na Pasipoti Gerald J. Kihinga, ametoa wito kwa Wananchi kuwa hakuna Uwakala katika huduma zinazotolewa na Idara ya Uhamiaji. Hivyo mtu anayeomba Pasipoti ya Tanzania au Vibali vya Ukaazi anatakiwa awasilishe maombi yake kupitia tofuti ya Idara ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni www.immigration.go.tz

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Kamishna wa Uhamiaji, Uraia na Pasipoti Gerald J. Kihinga, Kaimu Kamishna wa Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Paul Eranga pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Uratibu, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Peter G. Mbaku.

Bi. Praise akichangia hoja katika kikao hicho.


Bw. Mulokozi ambaye ni mjasiriamali katika moja ya vibanda vilivyo mkabala na Ofisi ya Uhamiaji akieleza utayari wake katika kukabiliana na tatizo la vishoka wakati wa kikao hicho






Kaimu Kamishna wa Usimaizi na Udhibiti wa Mipaka, naibu Kamishna Paul Eranga akiongea wakati wa kikao hicho


Kaimu Kamishna wa Uhamiaji, Kamishna Hannelore Manyanga akiongea wakati wa kikao hicho

Baadhi wa wafanyabiasha na wajasiriamali wanaofanya shughuli zao mkabala na jengo la Uhamiaji Makao Makuu Kurasini wakiwa katika kikao cha pamoja na Idara ya Uhamiaji ili kutafuta suluhu la Vishoka wanaotumia sehemu zao za biashara kama ofisi


Kamishna wa Uraia na Pasipoti, Kamishna Gerald Kihinga akiongea wakati wa kikao hicho