Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

11 Juni 2021

KAMISHNA WA UHAMIAJI ZANZIBAR AWATAKA WANANCHI KUFICHUA WAHAMIAJI WASIOFUATA SHERIA






Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari Masoud Sururu mapema wiki hii atembelea vipenyo mbali mbali katika Mkoa wa Kusini na Kaskazini Pemba ili kujionea mazingira halisi pamoja na kutoa elimu kwa Wananchi juu ya umuhimu wakushirikiana na Idara ya Uhamiaji katika kutoa taarifa kwa Wahamiaji wasiofuata sheria za Uhamiaji.

Akizungumza na Wananchi wanaoishi pembezoni mwa vipenyo vya mto wa kuwa na Mkia wa ng’ombe huko Kaskazini Pemba aliwataka wananchi kushiriki katika kuimarisha ulinzi kwenye vipenyo kwa kutoa taarifa kwa Idara ya Uhamiaji kuhusu chombo chochote kinachokusudia au kuonekana katika eneo hilo ili taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Kamishna Sururu aliwafahamisha Wananchi hao athari za Uhamiaji haramu ikiwa ni pamoja na kuhatarisha usalama wa nchi na Serikali kukosa mapato yatokanayo na malipo ya visa.

Aidha Wananchi walitaka kupatiwa elimu zaidi ya Uhamiaji ili wawe na uwezo wa kuwabaini Wahamiaji Haramu katika maeneo yao. Wananchi hao waliahidi kutoa mashirikiano na Idara ya Uhamiaji.

Nae Sheha wa Shehia ya Gando Maalim Karim Mangunja alibainisha kuwa hakuna vyombo vya kigeni vinavyoingia katika vipenyo hivyo hata hivyo aliahidi pale ikitokea chombo chochote ikitakachotiliwa shaka ataijuilisha Idara ya Uhamiaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni