Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

15 Desemba 2017

KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI AKUTANA NA WATANGULIZI WAKE

  • Achota busara hekima na ujuzi kutoka kwa wastaafu.
  • Wastaafu wamfagilia kwa utendaji kazi uliotukuka.
  • Wasema kwa sasa Idara inatekeleza kauli mbiu ya Mhe. Rais ya 'HAPA KAZI TU'.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala amepata fursa ya kukutana na viongozi waandamizi wastaafu waliowahi kuiongoza Idara ya Uhamiaji katika kikao cha pamoja kilichofanyika leo tarehe 15 Disemba 2017 katika Ukumbi wa Mikutano wa TEC, Kurasini jijini Dar es Salaam. 

Kikao kazi hicho kilikuwa na lengo la kupokea ushauri, kubadilishana mawazo na kupeana uzoefu baina ya viongozi wa sasa na viongozi waandamizi wastaafu wa Idara ya Uhamiaji.

Akifungua kikao hicho, Dkt Makakala alielezea furaha yake kwa kupata fursa ya kipekee kwa  kukutana na wazee ambao ni waanzilishi wa Idara ya Uhamiaji, na kuwaomba waweze kutoa ushauri wao na kubadilishana uzoefu na viongozi wa sasa wa Idara, juu ya masuala mbalimbali kwa nia ya kuongeza ufanisi na kutatua changamoto ambazo Idara imekuwa ikikabiliana nazo.

"Nina furaha kubwa sana yaani leo, sijui nieleze vipi. Leo nipo na Wakuu wangu walionilea idarani hadi na mimi nimekuwa Mkuu wa Idara. Ni jambo kubwa sana mmenifanyia kwa kukubali kuja hapa ili mnifunde mimi na wenzangu. Nawashukuru sana." alisema Kamishna Jenerali wa Uhamiaji wakati akiwakaribisha wastaafu hao.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wastaaafu, Mkurugenzi mstaafu wa Uhamiaji, Kinemo Kihomano alimpongeza Dkt Makakala kwa kuteuliwa kuwa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, na kumtaka kuendeleza yale mazuri yaliyoanzishwa na viongozi wastaafu na kuendeleza ubunifu na utekelezaji wa mipango mbalimbali aliyokwishaanza kuitekeleza kulingana na mahitaji ya wakati wa sasa.

Kwa upande wake Kamishna Ally Mnyika, mbali ya kumpongeza Dkt Makakala, alimshauri kufanya kazi bila woga wala upendeleo wa aina yoyote, kutekeleza na kusimamia maamuzi mbalimbali atakayokuwa akiyafanya ili mradi amezingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo.

Katika kikao hicho, viongozi mbalimbali wastaafu walipata fursa ya kutoa uzoefu wao juu ya masuala mbalimbali ya kiuhamiaji na namna walivyoweza kukabiliana na changamoto mbalimbali walizokutana nazo wakati wa uongozi wao  kwa nia ya kuboresha utendaji wa Idara ya Uhamiaji.

Ikumbukwe kwamba Idara ya Uhamiaji imepitia mabadiliko kadhaa ya vyeo vya uongozi ambapo hapo awali Mkuu wa idara alikuwa akijulikana kama Mkurugenzi wa Uhamiaji, baadae Kamishna Mkuu wa Uhamiaji na sasa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji.

Aidha katika Kikao hicho walihudhuria Wakurugenzi Wastaafu wa Uhamiaji Ally A. Mnyika, Judith Vicky Mtawali, Kinemo W. D. Kihomano na Magnus P. J Ulungi. Wengine ni Masauni Yusuf Masauni, Makame Usi Ali, na Ali Khamis Ali kwa upande wa Zanzibar. Kadhalika Makamishna Piniel O. Mgonja, Donald S. B. Ndagula, John Choma, Francis Kibula, Cuthbert Samba, Faustina B. Rutaihwa, Barikiel Shayo, George J. Kashwende pamaoja na Makamishna waliopo Madarakani kwa sasa na Viongozi Waandamizi wa Idara ya Uhamiaji kutoka Makao Makuu, Zanzibar pamoja na baadhi ya Mikoa walihudhuria.

Wakurugenzi wa Uhamiaji Wastaafu Ally A. Mnyika (kulia), Judith Mtawali (katikati) wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. A. P. Makakala akizungumza jambo wakati wa kikao kazi na watangulizi wake kilichofanyika leo jijini Dar es salaam.

Kamishna wa Uhamiaji Mstaafu Piniel O. Mgonja akichangia jambo katika kikao cha pamoja baina ya Viongozi Waandamizi Wastaafu wa Idara ya Uhamiaji na Viongozi Waandamizi waliopo madarakani.

Mkurugenzi Mkuu Mstaafu  wa Uhamiaji Zanzibar Masauni Yusuf Masauni akichangia hoja wakati wa kikao cha kubadilishana uzoefu wa kazi
Mkurugenzi Mstaafu wa Uhamiaji Judith Vicky Mtawali akizungumza wakati wa kikao cha kubadilishana uzoefu wa kazi baina ya Viongozi Waandamizi wastaafu wa Idara ya Uhamiaji na Viongozi Waandamizi wa Idara waliopo madarakani.

Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Idara ya Uhamiaji Kinemo Kihomano akizungumza wakati wa kikao cha kubadilishana uzoefu wa kazi baina ya Viongozi Waandamizi wastaafu wa Idara ya Uhamiaji na Viongozi Waandamizi wa Idara waliopo madarakani.

Picha ya pamoja ya Viongozi waandamizi wa  Idara ya Uhamiaji waliopo madarakani na Viongozi Waandamizi wastaafu wa Idara hiyo, wakati waliposhiriki katika kikao cha kubadilishana mawazo na uzoefu kilichoitishwa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt.  Anna Makakala.

Kamishna Wa Uhamiaji Zanzibar Johari Sururu akizungumza wakati wa Kikao hicho.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Uhamiaji Mzee Ally Mnyika.

Mamishna wa Uhamiaji Piniel O. Mgonja (kulia), John Choma (katikati) na Cuthbert Samba (kushoto) wakifuatilia yanayojili katika kikao hicho.

Manaibu Kamaishna wa Uhamiaji George J. Kashwende (kushoto), Francis Kibula (wapili kushoto), Faustina B. Rutaihwa na Barikieli Shayo wakifuatilia kikao hicho

Makamishna wa Uhamiaji Gerald Kihinga, Maurice D. Kitinusa, Mwinchum H. Salum na Mary Palmer wakifuatilia yanayojili katika kikao hicho.

Kamishna wa Uhamiaji Dkt. A. P. Makakala na Mkurugenzi Mstaafu wa Uhamiaji Judith Mtawali wakifuatilia yanayojili katika kikao hicho.



Makamishna wa Uhamaiji Kutoka kushoto Hannelore M. Mnyanga, Samwel R. Magweiga, Gerald Kihinga, na Maurice Kitinusa wakifuatilia yanayojili kwenye kikao hicho.

Makamishna wa Uhamiaji Maurice Kitinusa (kushoto), Mchinchum H. Salum(katikati) na Mary Palmer  (kulia) wakifuatilia yanayojili katika kikao hicho. 

Kamishna wa Uhamiaji Mstaafu Donald S. B. Ndagula akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Kamishna wa Uhamiaji Mstaafu Cuthbert Samba akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Kamishna wa Uhamiaji Mstaafu John Choma  akizungumza jambo kwenye kikao hicho.

Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Mstaafu Magnus P. J. Ulungi  akizungumza kwenye kikao hicho cha kubadilishana uzoefu na ushauri baina ya Viongozi Waandamizi Wastaafu na waliopo Madarakani.

Viongozi Waandamizi wa Idara ya Uhamiaji waliopo Madarakani na Wastaafu wakiwa katika picha ya pamoja kabala ya kunza kikao hicho.

Mkurugenzi  wa Uhamiaji Mstaafu Ally A. Mnyika akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Kamishna wa Uhamiaji Mstaafu Donald S. B. Ndagula akichangia jambo kwenye kikao hicho.

Kamishna wa Uhamiaji Donald S. B. Ndagula akichangia jambo kwenye kikao hicho

Mkurugenzi wa Uhamiaji Mstaafu  wa Zanzibar Masauni Yusuf Masauni akizungumza na waandishi wa habari baada kikao hicho.

Afisa Uhamiaji Mfawidhi wa Uthumishi, Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji Joseph Francis Kasike  akifuatilia jambo katika kikao hicho.

Kamaishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. A. P. Makakala akizungumza katika kiakao hicho.

Makamaishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari Sururu (kulia) na Makamishna wengine wakifuatilia kikao hicho

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni