Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

27 Desemba 2017

MATUKIO KATIKA PICHA: UHAMIAJI MKOA WA DODOMA WALIVYOSHIRIKI USAFI SAMBAMBA NA MKUU WA MKOA WA DODOMA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Dkt. Binilith Mahenge alivyoshiriki kufanya usafi katika Mtaa wa Zahanati Kata ya Kikuyu Kaskazini siku ya Jumamosi katika Kampeni ya Usafi wa Mji ambapo Watumishi wa Idara ya Uhamiaji walishiriki wakiongozwa na Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma Naibu Kamishna wa Uhamiaji P.J. Kundy.

Mkuu wa Mkoa Dkt. Binilith Mahenge akifanya usafi katika Kampeni ya Usafi wa Mji wa Dodoma.

Afisa Uhamiaji Mkoa Dodoma; Naibu Kamishna wa Uhamiaji P. J. Kundy akizungumza na waandishi wa Habari baada ya zoezi la Usafi wa Mji wa Dodoma.
Maafisa Uhamiaji wa Dodoma wakifanya Usafi katika Kampeni ya Usaifi wa Mji wa Dodoma


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma akiongea na waandishi wa Habari mara baada ya zoezi la Usafi wa Mji wa Dodoma

Baadhi ya Wananchi wa Dodoma walioshiriki katika siku ya usafi.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni