Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

06 Desemba 2017

Timu ya Netiboli ya Uhamiaji Queens yamaliza safari yake kwenye Ligi ya Muungano kwa ushindi wa Pili


Mabingwa mara mbili mfululizo wa Ligi Kuu ya Muungano mpira wa Pete, Timu ya Uhamiaji Queens imemaliza mashindano hayo kwa kushika nafasi ya pili nyuma ya timu ya Jeshi ya JKT Mbweni ambayo ilifanikiwa kushinda katika pambano la fainali kwa magoli 31-29, mjini Zanzibar.

Makamu Bingwa hao walipambana kwa udi na uvumba ingawa bahati haikuwa yao baada ya kutoka sare robo ya kwanza na kutofautiana kwa magoli mawili robo tatu za mwisho hivyo kulazimika kuuachia ubingwa ambao waliushikilia kwa muda wa miaka miwili mfululizo.

"Tumeshindwa kwa kupoteza pambano la leo, tupo tayari kupambana zaidi na kushinda fainali zilizo mbele yetu", alikiri kocha wa Uhamiaji Queens, Mkaguzi Msaidizi wa Magereza Winfrida Emmanuel.

Katika mechi za Makundi, Uhamiaji walianza kwa kuwabamiza Mafunzo mabao 40 kwa 39, wakacheza na Zimamoto nayo wakaibugiza magoli 64 kwa 27.

Mechi zingine walizocheza ni dhidi ya Jeshi Stars ambapo Uhamiaji waliibuka na ushindi wa mabao 56 kwa 49 ambapo mechi ya mwisho katika makundi walicheza na Duma ambapo waliwafunga magoli 61 kwa 29 na kufanikiwa kuingia nusu fainali.

Timu ya Uhamiaji Queens ilicheza fainali na timu ya KVZ ambapo malikia hao waliendeleza wimbi la ushindi kwa kuifunga timu hiyo mabao 55 kwa 43 na kufanikiwa kutinga fainali.

Katika mchezo wa fainali, Malikia hawa wa Uhamiaji pamoja na kucheza kwa ustadi mkubwa, Uhamiaji Queens walilazwa kwa bao 31 kwa 29 na kuambulia nafasi ya pili.

"Tumecheza vizuri sana ingawa JKT Mbweni wametuzidi kidogo ila nao wanajua Uhamiaji Queens ni timu ya vipi. Mashindano yajayo tutawadhibiti tu, kufungwa leo sio kwamba ndio watatufunga kila siku." Alisema Bi. Neema ambaye ni nahodha wa Uhamiaji Queens.

Uhamiaji Queens imekuwa ni kinara katika mashindano ya Netball hapa nchini na imekuwa ikileta sifa kubwa kwa idara ya Uhamiaji.


Nahodha akikabidhiwa Kombe la Mshindi wa Pili wa Michuano ya Netball nchini


Kikosi cha Timu na Benchi la Ufundi kilichotwaa nafasi ya pili ya Mashindano ya Netball nchini

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni