Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

21 Desemba 2017

SALAMU NA UJUMBE WA KRISMASI KWA WATANZANIA KUTOKA KWA KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI

Kamishna Jenerali Wa Uhamiaji kwa niaba ya Watumishi wote wa Idara ya Uhamiaji Tanzania anawatakia Watanzania Heri ya Krismasi na Mwaka Mpya wa 2018.

Aidha anatoa wito kwa wananchi wote hasa waishio maeneo ya mipakani kutoa taarifa kwa Idara ya Uhamiaji ama Vyombo vingine vya Dola pale wanapoona makundi ya watu wakipita katika maeneo yao, kwani Wahamiaji Haramu wanaweza kujipenyeza na kuingia nchini kipindi hiki cha Sikukuu za Mwisho wa Mwaka.

Pia anawakumbusha Watanzania kuwa, Uvushaji, ama Usafirishaji, Uhifadhi wa Wahamiaji Haramu au Usaidizi wa aina yoyote  kwa Wahamiaji ni Kosa la Jinai kwa Mujibu wa Sheria ya Uhamiaji


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni