Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

06 Desemba 2017

Uhamiaji Singida yaimarisha Doria na Misako ya Wahamiaji Haramu

Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Singida imeimarisha ukaguzi, doria na misako ili kudhibiti wahamiaji haramu; Doria na misako hiyo inajumuisha ukaguzi wa maghala, hoteli, maeneo ya starehe, magari ya mizigo pamoja na mabasi ya abiria.


Maafisa Uhamiaji wanaosimamia doria na misako wameonekana maeneo mbali mbali ndani na nje ya mji wa Singida wakitekeleza majukumu yao. Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji Elizabeth Kichonge ambaye alikuwa akiongoza kikosi cha Maafisa na askari watano alionekana akikagua nyaraka za wageni katika stendi ya mabasi ya mikoani mjini Singida.


“Kutokana na wimbi la wahamiaji haramu kubadili njia na sasa kupitia Mkoani kwetu kuelekea kusini mwa nchi, tumeamua kuzidisha ukaguzi kwenye vyombo vya usafiri. Kupitia zoezi hili, kuna mafanikio ambayo tumeyaona; mfano kwa siku chache hizi tulizofanya kazi, tumeshakamata watuhumiwa zaidi ya thelathini” Alisema Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Angela Shija ambaye ni Kaimu Afisa Uhamiaji Mkoa wa Singida.


Pamoja na ukaguzi, doria na misako inayoendelea kwa sasa, pia Uhamiaji Mkoa wa Singida wanatoa elimu ya Uhamiaji na Uraia kwa abiria wa mabasi, wananchi wa kawaida pamoja na vijana wanaoshiriki mafunzo ya Mgambo Mkoani humo. Pia Idara ya Uhamiaji Mkoani Singida inashirikiana kwa karibu na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) katika kufanikisha zoezi la uandikishwaji wa vitambulisho vya Taifa ili kuhakikisha watu wasiostahili hawajipenyezi kwa lengo la kuandikishwa.



Hadi sasa wahamiaji haramu 30 kutoka nchi za Maziwa Makuu (Rwanda, Burundi na DRC) tayari wameshakamatwa na hatua mbalimbali zimechukuliwa dhidi yao ambapo watu watano wamehalalisha ukaazi wao nchini, watu saba wameondoshwa nchini, watu 17 wanaendelea kuchunguzwa uhalali wa uwepo wao nchini na mmoja alifikishwa mahakamani na kukutwa na hatia ambapo alifungwa jela mwaka mmoja.



Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji Elizabeth Kichonge akikagua nyaraka za wageni katika stendi kuu ya mabasi yaendayo Mikoani.

Koplo wa Uhamiaji Faraja Wanjara akitoa elimu ya Uhamiaji na Uraia  kwa abiria  

Mkaguzi Msaidizi  wa Uhamiaji Isack Maganga (mwenye shati la draft) na Koplo wa Uhamiaji Abdallah Makacha wakiwateremsha watuhumiwa wa uhamiaji kwenye basi mara baada ya ukaguzi.

Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji Lawi Kumburu akimchukua maelezo mtuhumiwa alioingia nchini bila kibali cha Uhamiaji

Afisa Uhamiaji  akipekua  begi la mtuhumiwa 

Mkaguzi wa Uhamiaji Owden Kalengo na Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji Lawi Kumburu wakimuhoji mtuhumiwa ili kujiridhisha juu ya uraia wake.

Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji Roman Mtono akitoa elimu ya maswala ya Uhamiaji  kwa vijana wanaoshiriki mafunzo ya awali ya Mgambo. 


Wahamiaji Haramu waliokamatwa katika  kizuizi cha barabara kuu iendayo Dar Es Salaam 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni