Matangazo

📢 IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA — KARIBU KWENYE BLOG RASMI   ✦   📰 UHAMIAJI HABARI BLOGU — TUNAKULETEA MATUKIO KILA SIKU   ✦   📲 FUATA IDARA YETU KATIKA MITANDAO YA KIJAMII   ✦   ✉️ WASILIANA NASI: info@immigration.go.tz   ✦   ☎️ +255-22-2850575/6

12 Desemba 2017

UHAMIAJI ILIVYOSHIRIKI SHEREHE ZA MIAKA 56 YA UHURU WA TANZANIA BARA

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna P. Makakala aliungana na Wakuu wa Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama nchini kuadhimisha sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara ambazo zilifanyika tarehe 9/12/2017.

 Kwa mara ya kwanza Sherehe za Uhuru zikifanyika mkoani Dodoma, Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli amewaongoza Maelfu ya  Wananchi kwenye sherehe  hizo zilizofanyika katika uwanja wa Jamhuri.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji pamoja na Maafisa Waandamizi wa Uhamiaji waliungana na Wakuu wengine wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama  katika Sherehe za Miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara.

Sherehe hizo zilianza majira ya saa mbili asubuhi ambapo kama ilivyo taratibu za kiitifaki, Viongozi wakuu wa Serikali na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama (akiwemo Kamishna Jenerali wa Uhamiaji) waliongozwa na Makamu wa Rais kumlaki Amiri Jeshi Mkuu.

Sherehe hizo pia zilihudhuriwa na marais wastaafu wa Awamu ya Pili (Mhe. Ally Hassan Mwinyi), Tatu (Mhe. Benjamin W. Mkapa) na Nne (Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete) zilipambwa na gwaride na maonesho mbalimbali kutoka vikosi mbalimbali vya majeshi ya ulinzi na usalama.












Hakuna maoni:

Chapisha Maoni