Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna P. Makakala aliungana na Wakuu wa Vyombo vingine
vya Ulinzi na Usalama nchini kuadhimisha sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa
Tanzania Bara ambazo zilifanyika tarehe 9/12/2017.
Kwa mara ya kwanza Sherehe za Uhuru
zikifanyika mkoani Dodoma, Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Rais Dkt.
John Magufuli amewaongoza Maelfu ya Wananchi
kwenye sherehe hizo zilizofanyika katika
uwanja wa Jamhuri.
Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji pamoja na Maafisa Waandamizi wa Uhamiaji waliungana na
Wakuu wengine wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama
katika Sherehe za Miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
Sherehe
hizo zilianza majira ya saa mbili asubuhi ambapo kama ilivyo taratibu za
kiitifaki, Viongozi wakuu wa Serikali na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama
(akiwemo Kamishna Jenerali wa Uhamiaji) waliongozwa na Makamu wa Rais kumlaki
Amiri Jeshi Mkuu.
Sherehe
hizo pia zilihudhuriwa na marais wastaafu wa Awamu ya Pili (Mhe. Ally Hassan
Mwinyi), Tatu (Mhe. Benjamin W. Mkapa) na Nne (Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete)
zilipambwa na gwaride na maonesho mbalimbali kutoka vikosi mbalimbali vya
majeshi ya ulinzi na usalama.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni