Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

05 Februari 2020

Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Atembelea Ofisi ya Uhamiaji


Dar es salaam
Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza (CGP) Suleiman Munyiya Mzee leo amefanya ziara ya kujitambulisha katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam na kupokelewa na Mwenyeji wake Kamishna Jenerali wa Uhamiaji (CGI) Dkt. Anna Peter Makakala.

Akizungumza mara baada ya kufika katika Ofisi hiyo Kamishna Jenerali Mzee ameiomba Idara ya Uhamiaji kumpatia ushirikiano wa kutosha katika uongozi wake ili kusimamia vyema maelekezo yaliyotolewa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa Jeshi hilo ikiwemo jukumu la kujitegemea kwa chakula cha wafungwa na kuhakikisha Jeshi hilo linakuwa na miradi mingi ya uzalishaji mali na yenye tija.

“Kwa kweli mimi sikutegemea kupata uteuzi huu, nilikuwa Mkuu wa Kamandi kule Pangawe (Morogoro) lakini Mhe. Rais akaona nafaa kuja kulitumikia Taifa kupitia Jeshi la Magereza namshukuru sana" alisema Kamishna Jenerali Mzee.

Aidha, amewashukuru wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa ushirikiano wanaompatia katika kutimiza adhma ya Mhe. Rais ya kutaka kuona Jeshi la Magereza linajitegemea kwa chakula.

Kwa upande wake Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala amempongeza Kamishna Jenerali wa Magereza Suleiman Mzee kwa kuaminiwa na Mhe. Rais kuliongoza Jeshi la Magereza na amemtakia mafanikio mema katika majukumu yake mapya na kumuahidi ushirikiano wa kutosha ili kufikia malengo ya uchumi wa Taifa kwa faida ya kizazi cha sasa na baadae.

Ikumbukwe kuwa Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Suleiman Mzee aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 31 Januari 2020 akichukua nafasi ya aliyekuwa Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

HABARI PICHA NA MATUKIO
Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza (CGP) Suleiman Munyiya Mzee akiwasili katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam

Askari wa Uhamiaji wakitoa Salamu ya Heshima kwa Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza (CGP) Suleiman Munyiya Mzee 
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala akimpokea Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Suleiman Munyiya Mzee alipowasili katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam. 
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar  Johari Masoud Sururu akisalimiana na Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Suleiman Munyiya Mzee alipowasili katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam.

Kamishna wa Uhamiaji wa Divisheni ya Vibali vya Ukaazi, Visa na Pasi Mary Palmer (ndc) akisalimiana na Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Suleiman Munyiya Mzee alipowasili katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam.
Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Suleiman Mzee akisaini Kitabu cha Wageni ofsini kwa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji






Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala akimkabidhi Jarida la Uhamiaji Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Suleiman Munyiya Mzee alipowasili katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam. 

Picha ya Pamoja


 Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Suleiman Munyiya Mzee (Kulia) na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala wakiteta jambo wakati wa kuagana katika Ofisi ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam.



(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni