Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

16 Septemba 2020

CGI Dkt. Anna Makakala Atoa Maagizo kwa Maafisa Uhamiaji Mikoa Yote Nchini Kuwa na Maafisa Uhamiaji Kata.

Kigoma, Tanzania

Kamishna Jenerali wa uhamiaji nchini Dkt. Anna Makakala ametoa maagizo hayo Mkoani Kigoma akiwa katika ziara ya Kikazi ya Kukagua mipaka ya nchi na kukagua utendaji kazi wa Maafisa na Askari wa Uhamiaji ambapo amewataka Maafisa Uhamiaji Mikoa kote nchini kuhakikisha wanatekeleza agizo la kuwa  na Maafisa Uhamiaji Kata kwa kila kata kote nchini ili kusogeza  huduma karibu kwa wananchi.

“Niwatake Maafisa Uhamiaji kote nchini kuhakikisha mnatekeleza magizo haya na pia kutoa mawasiliano kwa wanachi ili waweze kufikisha shida zao na pia kusaidia kutoa taarifa za wahamiaji haramu katika maeneo yao ili tukomeshe kabisa suala la wahamiaji haramu” alisema

Aidha amewataka pia kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya Kiuhamiaji kwa kutumia njia mbalimbali  zikiwemo za televisheni redio, Magazeti Mikutano na warsha mbalimbali.

Hata hivyo CGI Dkt. Anna Makakala ameelekeza pia Maafisa na askari kuendelea kufanya kazi kwa, utii uhodari, uzalendo, Uwajibikaji na kwa weledi wa hali ya juu sanjari na kuwa na upendo, mshikamano na ushirikiano na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ili kuhakikisha ulinzi na Usalama Mipakani Unaimarishwa Ipasavyo kwa kufanya doria na misako ya mara kwa mara hasa wakati huu wa Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani.

Aidha ametoa rai kwa wananchi wote kushirikiana na vyombo vya ulinzi na Usalama katika Kuilinda mipaka ya nchi sanjari na kuwahakikishia Wananchi wa Kigoma katika kuongeza kasi ya Kuwahudumia ili waweze  Kupata vitambulisho vya Taifa kwa wakati hasa kwa Kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA. 

Akitoa taarifa ya Utendaji kazi ya Mkoa wa Kigoma, Afisa Uhamiaji Mkoa Naibu Kamishna wa Uhamiaji (DCI) Remigius Pesambili amesema katika kupunguza wimbi la uhamiaji haramu Mkoani Kigoma Mkoa umekuwa ukifanya Misako doria na operesheni katika maeneo mbalimbali ambapo kwa kipindi cha mwezi Julai 2019 mpaka Agosti 2020 wamekamatwa wahamiaji haramu 5576 na kuchukuliwa hatua stahiki kwa mujibu wa sheria ikiwepo kufikishwa Mahakamani na wengine kurudishwa nchini kwao.

Akiongelea Mikakati ya Kudhibiti wahamiaji haramu DCI Pesambili amesema kwamba Mkoa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kigoma inatekeleza mkakati wa kutokomeza kabisa wimbi la wahamiaji haramu kwa kuendelea na misako na doria, Kimarisha Vizuizi vya barabarani katika maeneo yote ya kimkakati, kuimarisha mpango wa utoaji elimu ya uraia  na athari zitokanzo na uingiaji  wa wahamiaji haramu sanjari na kuanzisha mpango wa kugawa kata  kwa kila Afisa Uhamiaji ili kusogeza huduma karibu na wananchi na kusaidia kudhibiti wimbi la wahamiaji haramu kuanzia ngazi ya chini mpaka juu.

Katika kuhakikisha shughuli za Uhamiaji katiaka Mkoa wa Kigoma zinatekelezwa kwa ufanisi  na kudhibiti uhamiaji haramu  Mkoa umeomba kupatiwa mafunzo ya mara kwa mara ambayo hasa yanahusiana na msuala ya Intelejensia Katika Udhibiti wa mipaka.

Katika ziara yake Kamishna Jenerali Wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala ametembelea karibu wilaya zote za Mkoa wa Kigoma ikiwemo Wilaya ya Kakonko, Kibondo, Kasulu Buhigwe, Kigoma Mjini na vituo vya Uhamiaji vya kutoka na kuingia nchini vikiwemo vituo vya Mabamba , Manyovu, Kibirizi, Ujiji, Bandari ya Kigoma  na Kibirizi.

 HABARI PICHA NA MATUKIO

Kamishna Jenerali wa uhamiaji nchini Dkt. Anna Makakala akiwa katika Picha ya pamoja na Askarina watumishi wa Uhamiaji katika Ofisi ya Mkoa Kigoma


Kamishna Jenerali wa uhamiaji Dkt. Anna Makakala akiwa katika Picha  ya pamoja na Maofisa na Askari wa Uhamiaji Wilaya ya Kasulu

 Afisa Uhamiaji Mkoa Naibu Kamishna wa Uhamiaji (DCI) Remigius Pesambili Akitoa taarifa ya Utendaji kazi ya Mkoa





Kamishna Jenerali wa uhamiaji nchini Dkt. Anna Makakala akisalimiana na Askari wa Uhamiaji Wilaya ya Kasulu



(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni