Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

11 Septemba 2020

CGI Dkt. Anna Makakala Awataka Maafisa na Askari wa Uhamiaji Kuongeza Uhodari na Weledi zaidi katika Kutoa Huduma za Kiuhamiaji.

Dar es salaam

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini (CGI) Dkt. Anna Makakala mapema wiki hii amefanya ziara ya kikazi katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es salaam na kufanya kikao na Maafisa na Askari wa Uhamiaji katika Kituo hicho.

Akiongea uwanjani hapo CGI Dkt. Makakala amesema kwamba Idara ya Uhamiaji iko macho muda wote katika ulinzi wa mipaka yote ya nchi ikiwemo katika uwanja huo ambao ni lango la kuingilia nchini (Entry Point)

“Zingatieni  Maadili na Misingi ya kazi yenu, huku mkiongeza Umakini Uhodari Uaminifu na Weledi katika kutoa huduma za kiuhamiaji zenye viwango vya kitaifa na kimataifa sanjari na  kuendelea na  juhudi za Ulinzi na Usalama hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani” alisema

Aidha amewakumbusha Maofisa na Askari kuendelea kuishi katika kauli mbiu ya Uhamiaji yenye Upendo Mshikamano Uwajibikaji na Kukataa Rushwa, ili kuwezesha kudhibiti uingiaji na utokaji wa watu kupitia utekelezaji wa sheria na kanuni zilizopo  ili kulinda Usalama wa Taifa na kukuza Maendeleo ya Kiuchumi.

Kwa upande wake Kamishna wa Uhamiaji Uraia na Pasipoti Gerald Kihinga amewaeleza pia Maafisa na askari juu ya maendeleo mazuri ya Ujenzi wa chuo cha Uhamiaji Kinachojengwa huko Wilayani Mkinga Mkoani Tanga ambapo amemshukuru Kamishna Jenerali Dkt. Anna Makakala kwa kuwa na dira ya kuanzisha chuo hicho kwa ajili ya mafunzo ya Maafisa na Askari kwa ngazi zote.

Mfawidhi Mkuu wa Kituo cha Uhamiaji Katika Uwanja huo Naibu Kamishna wa Uhamiaji DCI Albert Rwelamira amemhakikishia Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala kwamba wataendelea kutoa huduma zenye kiwango cha kitaifa na Kimataifa kwa utii uhodari, uzalendo na weledi wa hali ya juu ili kufikia malengo ya Idara na Taifa kwa ujumla.

HABARI PICHA NA MATUKIO
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini CGI Dkt. Anna Makakala

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini (CGI) Dkt. Anna Makakala Akiongea na Maofisa na Askari wa Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa (JNIA)


Baadhi ya Maafisa na Askari wakimsikiliza kwa Makini Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini (CGI) Dkt. Anna Makakala

Askari wa Uhamiaji JNIA 


Kamishna wa Pasipoti na Uraia Gerald Kihinga akiongelea kuhusu suala la maendeleo ya ujenzi wa  chuo kipya cha Mafunzo kwa maafisa na askari wa Uhamiaji








Mfawidhi Mkuu wa Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa ndege wa Kimataifa JNIA Naibu Kamishna wa Uhamiaji (DCI) Albert Rwelamira akitoa Taarifa fupi ya utendaji kazi kwa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini (CGI) Dkt. Anna Makakala




(Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu )

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni