Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

18 Desemba 2019

NAIBU WAZIRI MASAUNI AHITIMISHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHAMAJI DUNIANI










































Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni leo tarehe 18/12/2019 amehitimisha maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wahamaji katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Uhamiaji Kurasini Dar Es Salaam. Maadhimisho hayo ambayo yanafanyika kila mwaka yanalenga kutambua haki za wahamaji pamoja na familia zao wanapokuwepo katika nchi za kigeni.

Akihutubia katika Maadhimisho hayo Mheshimiwa Masauni amempongeza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala kwa kufanya mabadiliko makubwa kwenye Mifumo ya kutolea huduma zake kwa njia ya Mtandao ambapo sasa mgeni anaweza kuomba Visa au Vibali vya Ukaazi, kufanya malipo pamoja na kupokea kibali chake kwa njia ya mtandao akiwa mahali popote Ulimwenguni bila ya kulazimika kufika katika Ofisi za Uhamiaji.

Aidha, Naibu Waziri aliongeza kuwa Serikali imefanya marekebisho ya Sheria ya Uhamiaji kwa kuanzisha vibali maalumu vya ukaazi kwa wahamiaji walowezi walioo hapa nchini ili kutatua tatizo la uhamiaji haramu nchini. Pia Serikali imepunguza ada ya kibali cha Ukaazi kwa wawekezaji wan je wenye asili ya Tanzania (Diaspora) kutoka Dola za Kimarekani 3050 hadi kufikia Dola 1000 ili kuhamasisha raia hao kuwekeza katika nchi yao ya asili.

Awali akimkaribisha Naibu Waziri Masauni, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala ameeleza kuwa kwa sasa Idara ya Uhamiaji inaendelea kuzifanyia kazi changamoto zinazo wakabili wateja wa huduma za Uhamiaji.

Dkt. Makakala aliongeza kuwa kutokana na maboresho hayo, Waombaji wa huduma za Uhamiaji hususani  Pasipoti hawatalazimika kuwasilisha katika Ofisi za Uhamiaji Viambata vya nakala halisi watakapo hitaji Pasipoti. Badala yake Viambato hivyo vitatakiwa kuwasilishwa kwa njia ya Mtandao pekee.

Katika Maadhimisho hayo Idara ya Uhamiaji na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) wamesaini Makubaliano ambayo yatawezesha mifumo ya huduma ya Taasisi hizo mbili kupeana taarifa muhimu ikiwemo cheti cha kuzaliwa ambacho ni mojawapo ya kiambata muhimu wakati wa kuomba Pasipoti.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni