Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

31 Desemba 2019

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Afanya Ziara ya Kushitukiza Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Nyerere. (JNIA)


Dar es salaam

Kamishina Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala leo amefanya ziara ya kushitukiza katika kituo cha Uhamiaji cha uwanja wa ndege wa Kimataifa wa  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JNIA) jijini Dar es salaam ikiwa ni lengo la kukagua utekelezaji wa Shughuli za uhamiaji katika kituo hicho.
Akifanya Kikao na Watumishi kituoni hapo Dkt.Makakala amewataka watumishi wote wanaofanya kazi katika kituo hicho kufanya kazi kwa nidhamu, utii, uhodari, na weledi  na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ikiwemo kutojihusisha na masuala ya rushwa.
Aidha ameapa kutowavumilia maafisa askari na watumishi wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na kwamba atawachukulia hatua kali za kinidhamu ikiwemo kuwafuta kazi na kuwafikisha mahakamani.
Sanjari na hilo amesisitiza pia kuongeza juhudi za ukusanyaji maduhuli ya serikali ili kuongeza pato la taifa na kuchochea maendeleo kwa faida ya kizazi cha sasa na baadae.
Ili kuongeza ufanisi zaidi katika utekelezaji wa majukumu ya ulinzi na usalama wa nchi kupitia mipaka na njia zote za kuingilia na kutokea  nchini, Dkt. Makakala amewataka maafisa na askari wote kushirikiana na vyombo vyote vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha nchi inakuwa salama.
Ziara ya Kamishina Jenerali ni muendelezo wa ziara za mara kwa mara katika kukagua shughuli za utendaji kazi ili kuhakikisha idara  inafikia malengo yake mahususi ya utendaji kwa  kutoa huduma za uhamiaji zenye kukudhi viwango vya kitaifa na kimataifa. 

HABARI NA MATUKIO

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala Akitoa Maelekezo kwa Maofisa, Askari na watumishi wa Uhamiaji katika Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere  (JNIA) Jijini Dar es salaam.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala Akitoa Maelekezo kwa Maofisa, Askari na watumishi wa Uhamiaji katika Kituo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JNIA) Jijini Dar es salaam.

Baadhi ya Maofisa na Askari wa Uhamiaji Kituo cha Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es salaam wakimsikiliza kwa makini Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala (Hayupo Pichani) 
Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Makao Makuu ya Uhamiaji

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni