Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

02 Desemba 2019

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AFUNGUA MKUTANO WA UHAMIAJI NA WADAU WA HUDUMA ZAKE

Mkuu wa Wilaya ya Karatu Bi. Theresia Mahongo (katikati) akiwa na Afisa Uhamiaji Mkoa Arusha Naibu Kamishna wa Uhamjia Abdallah Towo (kushoto) na Kamishna wa Uhamiaji -Vibali na Pasi Mary Palmer wakati wa mkutano wa Idara ya Uhamiaji na wadau wa huduma za kiuhamiaji.

Wadau wa huduma za Uhamiaji waliohudhuria mkutano huo katika Ukumbi wa Mount Meru Hotel jijini Arusha.







Mkutano wa Idara ya Uhamiaji na Wadau wa Huduma za Uhamiaji mkoa wa Arusha umefanyika leo tarehe 2 Disemba 2019 katika Ukumbi wa Mount Meru Hotel jijini Arusha. Mgeni rasmi wa mkutano huo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo aliyewakilishwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Bi. Thresia Mahongo.


Lengo la mkutano huo ni kuwakutanisha Wadau wa huduma za Uhamiaji Mkoani Arusha na kuwajengea uelewa juu ya masuala mbalimbali ya Kiuhamiaji, hususani huduma za Kielektroniki; pamoja na kupokea maoni kutoka kwa wadau hao ili kutatua changamoto mbalimbali na kuboresha huduma za Uhamiaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni