Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

27 Desemba 2019

Uhamiaji yamlilia Ngonyani

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala jana tarehe 26 Disemba 2019 ameongoza waombolezaji waliohudhuria ibada ya kumuaga Kamishna Msaidizi Mwandamizi mstaafu Sylvester Peter Ngonyani aliyefariki usiku wa kuamkia tarehe 25 Disemba 2019.

Ibada hiyo ilifanyika nyumbani kwa marehemu Toangoma Kigamboni, ambapo mbali na kuhudhuriwa na Kamishna Jenerali, Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha, Maafisa Waandamizi wa Uhamiaji, Maafisa, askari na watumishi wengine wa Uhamiaji walihudhuria katika ibada hiyo.

Marehemu Sylvester Peter Ngonyani aliajiriwa Idara ya Uhamiaji mwaka 1990

Marehemu alizaliwa  tarehe 09 Disemba 1964 katika Kijiji cha Ngoheranga wilayani Malinyi Mkoa wa Morogoro, alisoma shule ya msingi Ngoheranga baadaye Kibasila na Shycom kwa elimu ya sekondari. Pia elimu ya juu aliipata Chuo Kikuu cha Mzumbe. Aliajiriwa na Idara ya Uhamiaji Mwaka 1990, na kushika nyadhifa mbalimbali mpaka anastaafu mwishoni mwa mwaka huu marehemu Ngonyani alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Anuai za Jamii Makao Makuu ya Uhamiaji. Marehemu ameacha Watoto watano na wajukuu wawili. Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina lake Lihimidiwe.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akitoa heshima zake kwa Marehemu Sylvester Ngonyani 


Kamishna wa Uhamiaji (Utawala na Fedha) Edward Chogero akitoa neno kwa niaba ya Uhamiaji


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni