Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

17 Desemba 2019

JENERALI MABEYO AFUNGA MAFUNZO KWA ASKARI WA UHAMIAJI
























































Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo leo Jumanne Disemba 17, 2019 amefunga rasmi mafunzo ya Awali kwa askari wapya 400 wa Idara ya Uhamiaji, hafla ambayo imefanyika katika Chuo cha Uongozi cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kimbiji mkoa wa Pwani.


Akizungumza katika hafla hiyo, Jenerali Mabeyo amewataka Asakari hao kufanya kazi kwa Uzalendo na kutii kiapo walichoapa leo kwa kutimiza majukumu yao kwa weledi huku wakizingatia Sheria, Kanuni na Taratibu za Uhamiaji.


"Serikali imewaamini na kuwapatia dhamana kubwa hivyo kuweni wazalendo na waadilifu wakati mnapowahudumia Wananchi"alisema Jenerali Mabeyo.


Pia Jenerali Mobeyo amempongeza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya kufanya mabadiliko ndani ya Uhamiaji na mahusiano mazuri yaliyopo na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama, akitolea mfano namna Idara ya Uhamiaji inavyoshughulikia maombi ya pasipoti kwa Maafisa na Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wanaokwenda nje ya nchi kulinda amani.


Awali akimkaribisha Jenerali Mabeyo, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala alimshukuru Jenerali Venance Mabeyo kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika hafla ya kufunga mafunzo hayo pamoja na kuwa anayo majukumu mengi ya kitaifa.


Mafunzo hayo ya Awali kwa Askari wa Idara ya Uhamiaji ya Awamu ya Kwanza kwa Mwaka huu yalifunguliwa tarehe 23 Septemba,  2019 na yamehitimishwa leo yamejumuisha Askari wanaume 326 na wanawake 74.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni