Visitors
29 Machi 2018
26 Machi 2018
ANATAFUTWA
NDG. FAISALI HIRARY MWENYE PICHA HAPO JUU ANATAFUTWA NA
IDARA YA UHAMIAJI KWA KOSA LA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU KINYUME NA KIFUNGU
CHA 46 CHA SHERIA YA UHAMIAJI, SURA YA 54, REJEO LA MWAKA 2016.
YEYOTE
MWENYE TAARIFA KUHUSU MTUHUMIWA HUYO, ANAOMBWA KUIFIKISHA KATIKA OFISI YOYOTE
YA UHAMIAJI AU KITUO CHA POLISI KILICHO KARIBU NAYE.
AIDHA,
TAARIFA INAWEZA KUTOLEWA KWA NJIA YA SIMU KUPITIA NAMBA IFUATAYO: 0768
636 505.
“Pamoja Tushirikiane Kuilinda Nchi Yetu”
-------------------------
IMETOLEWA
NA
KITENGO CHA UHUSIANO,
IDARA
YA UHAMIAJI,
MAKAO MAKUU,
16 Machi 2018
07 Machi 2018
ELIMU KWA UMMA SINGIDA YAZAA MATUNDA, WATUHUMIWA SITA WAKAMATWA
Idara ya Uhamiaji Mkoani Singida
imetoa elimu kwa Umma kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Idara ya
Uhamiaji zikiwemo Pasipoti, Vibali vya Ukaazi,Uraia na Uhamiaji haramu. Zoezi
hilo linaendelea kufanyika katika Wilaya zote Sita za mkoa wa Singida ambazo ni Manyoni, Mkalama, Ikungi, Iramba,
Singida Mjini na Vijijini.
Katika kutekelaza zoezi hilo
Maafisa Uhamiaji Wilaya wanashirikiana na Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya
husika pamoja Maafisa Watendaji wa Kata na Mitaa/Vitongoji mbalimbali ikiwa ni
lengo la kuwajengea uelewa Viongozi hao kuhusu masuala yanayohusu Uhamiaji.
Sambamba na elimu kwa umma,
Uhamiaji Singida wameimarisha Mapambano ya Wahamiaji haramu kwa kufanya misako
na doria za mara kwa mara katika maeneo yanayozaniwa kuwa hifadhi ya Wahamiaji
haramu.
“Mpango huu wa Elimu kwa Umma umesaidia
kufanikisha kuwakamata Wahamiaji haramu [02] Raia wa Ethiopia pamoja na Watanzania [04]
ambao wanajihusisha na biashara haramu ya kusafirisha Wahamiaji haramu, Watuhumiwa
wote wamefikishwa Mahakamani. Wananchi wamekuwa na mwamko na wamesaidia katika kuwaafichua watuhumiwa hao. Natoa rai kwa Wananchi kuendelea kushirikiana na Idara ya
Uhamaji kwa kutoa taarifa kwa Vyombo vya ulinzi na usalama pale wanapobaini
kuna mtu au kikundi cha watu wanaodhaniwa kuwa wahamiaji haramu’’ alizungumza
Kaimu Afisa Uhamiaji Mkoa Singida, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Angela M. Shija.
Katika zoezi hilo kwa Wilaya ya
Iramba inaongozwa na Kaimu Afisa Uhamiaji Wilaya Mkaguzi Dotto Selasini na kwa Wilaya
za Singida Mjini na Vijijini linaratibiwa na kusimamiwa na Wakaguzi Wasaidizi
Lawi Kumburu na Marcelin Marwa. Fuatilia habari picha zifuatazo:-
![]() |
Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe. Emmanuel Lwehaula (aliyeshika kitabu) akiwa na viongozi mbalimbali wa wilaya katika mkutano ambapo Kaimu Afisa Uhamiaji alipata fursa ya kutoa elimu kwa Umma.
|
![]() |
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Kidaru waliohudhuria mkutano ambapo walipata elimu katika masuala mbalimbali yanasimamiwa na Idara ya Uhamiaji.
|
![]() |
Wanakijiji wa Kidatu wakifuatilia kwa makini Elimu juu wa Wahamiaji Haramu iliyokuwa ikitolewa na Mkaguzi wa Uhamiaji Dotto Selasini
|
06 Machi 2018
Uhamiaji walipotia 'Mguu' Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala cha jijini Dar
Ukaguzi wa uhalali wa Ukaazi wa watumishi wa chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala uliofanywa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akiwa na Mheshimiwa Waziri wa Elimu Prof. Joyce Ndalichako chuoni hapo Gongolamboto jijini Dar es salaam.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)