Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

30 Agosti 2019

WAZIRI LUGOLA KUFUNGUA MKUTANO WA MAAFISA UHAMIAJI WAANDAMIZI


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Kangi Lugola kesho Jumamosi tarehe 31 Agosti anatarajiwa kufungua mkutano wa Maafisa Uhamiaji Waandamizi kutoka mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar.  

Akitoa taarifa hiyo mjini Moshi leo, Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Mrakibu Mwandamizi Alhaji Ally Mtanda amesema kuwa mkutano huo wa siku mbili chini ya Uenyekiti wa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala utafanyika katika Chuo cha Kikanda cha Uhamiaji (TRITA) mjini Moshi una lenga kujadili na kutathmini utendaji kazi wa idara pamoja na kukumbushana masuala mbalimbali hususan Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na raia wa kigeni.

“Mkutano huu utahudhuriwa na Makamishna wa Uhamiaji, Maafisa Uhamiaji Mikoa yote Tanzania na Zanzibar, Wakuu wa Vitengo pamoja na Wafawidhi wa Vituo vya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA), Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), Namanga, Tunduma na Bandari ya Zanzibar.” Aliongeza Alhaji Mtanda.  




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni