Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

26 Mei 2020

ACI Mwanjotile afanikiwa kusambaratisha wahamiaji haramu Mtwara


Mtwara,Tanzania Aliyekuwa Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi (ACI) James A. Mwanjotile mapema wiki hii akikabidhi ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mtwara kwa Kamishna Msaidizi Novati Dawson Kato alisema moja ya mafanikio yake makubwa anayojivunia wakati wa uongozi wake Mkoani hapo ni kupambana na kupunguza wimbi la wahamiaji haramu kwa kushirikiana na Wananchi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ambapo mpaka sasa hali ya Mkoa huo ni shwari.


Ameyasema hayo wakati wa makabidhiano ya ofisi ya uhamiaji Mkoa wa Mtwara mara baada ya Kamishina Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala kufanya mabadiliko madogo ya uongozi ndani ya Mkoa huo ambapo amemuhamisha Kamishina Msaidizi James A. Mwanjotile kwenda Jijini Dodoma Kuwa Afisa Uhamiaji Mkoa kuchukua nafasi ya aliyekua Afisa Uhamiaji jijini hapo  Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACI) Abdallah Kitimba ambae amestaafu kazi kwa mujibu wa sheria.

Mabadiliko hayo yameambatana na uteuzi wa Afisa Uhamiaji mpya wa Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi Novati Kato ambaye awali alikuwa Afisa Uhamiaji Msaidizi Mkoa wa Morogoro.

Akikabidhi Ofisi, Rasilimali watu na vifaa Kamishina Msaidizi Mwanjotile amewashukuru maofisa na askari wa Mkoa huo kwa kumpa ushirikiano wa kutosha kwa kipindi chote alichoongoza Mkoa huo na kuwataka kuendeleza ushirikiano huo kwa kiongozi mpya aliyewasili kuchukua nafasi yake.

Kamishina Msaidizi James A. Mwanjotile anaondoka Mkoa wa Mtwara akiwa amehudumu kwa kipindi cha miaka mitatu (3) Kwa nafasi hiyo ya Afisa Uhamiaji Mkoa na kuleta na mafanikio makubwa sana kwa Taifa, kutokana na Uongozi wake imara wenye Utii, Uhodari na Weledi wa hali ya juu.

HABARI PICHA NA MATUKIO


Aliyekuwa Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi (ACI) James A. Mwanjotile (katikati) akiongoza kikao cha makabidhiano ya Ofisi kwa  Afisa Uhamiaji mpya wa Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi Novati Kato (wa kwanza kulia) wengine ni Maafisa na Askari wa Uhamiaji Mkoani hapo 

Kaimu Afisa Uhamiaji Wilaya ya Tandahimba Mkaguzi Msaidizi Raymund Mapunda (Aliyesimama) akitoa maelezo ya awali kuhusu kituo cha Uhamiaji wilayani hapo
Mfawidhi wa Kituo cha Mtambaswala kilichopo wilaya ya Nanyumbu Mkoani Mtwara Mkaguzi Emmanuel Mtosa (Kushoto) akitoa maelezo ya Mpaka wa Tanzania na Msumbiji katika daraja la Umoja wakati wa makabidhiano ya ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mtwara

Makabidhiano ya Ofisi za Vituo Mbalimbali vya Uhamiaji yakiendelea






Mfawidhi wa Kituo cha Uhamiaji Kilambo Mkaguzi Nestori Riwa (Kushoto) akitoa maelezo ya kituo wakati wa Makabidhiano kituo hicho kipo Wilaya ya Mtwara Vijijini Mkoani Mtwara


(Picha zote na Ofisi ya Uhusiano Uhamiaji Mkoa wa Mtwara)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni