Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

16 Mei 2020

RC Ruvuma Akagua Utayari wa Idara ya Uhamiaji Mipakani

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Christina S. Mndeme mapema wiki hii amefanya ziara ya  kutembelea vipenyo vya mkoa Ruvuma kukagua utayari wa Idara ya Uhamiaji na vyombo vya ulinzi  na Usalama kwa ujumla katika  kukabiliana na wahamiaji haramu hasa wakati huu wa Mapambano dhindi ya ugonjwa w Covid -19 unaosababishwa na Virusi vya Corona.

Ziara hiyo imemfikisha Mkuu wa Mkoa na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama Wilayani Nyasa katika kipenyo cha Chiwindi kinachopakana na nchi jirani ya Msumbiji. 

Lengo kuu la ziara hiyo kufanyika  ilikuwa ni kujiridhisha na ulinzi na usalama mipakani ili kudhibiti matukio yoyote yanayoweza kutokea hasa wakati huu ambapo wengi wanaweza kutumia fursa hiyo kufanya vitendo vya kihalifu kama vile matishio ya kiusalama (ugaidi), usafirishaji wa wahamiaji haramu kwa njia za (Panya) vipenyo nk.

Aidha Mhe. Mndeme ameipongeza Idara ya Uhamiaji kwa kufanya kazi zake kwa makini katika mipaka hiyo na kusisitiza kuendelea kufanya doria za mara kwa mara na kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ili kuhakikisha ulinzi  na usalama wa Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla unaimarishwa wakati wote.

Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi wa maeneo hayo ya mipakani  kuendelea kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutoa taarifa pale wanapoona wageni wasiowafahamu kuingia chini au wanapoona vitendo viovu vyovvote vinapotokea ambavyo ni kinyume na sheria basi watoe taarifa, kwani jukumu la kuilinda nchi ni la kila Mtanzania. 

HABARI PICHA NA MATUKIO
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Christina S. Mndeme akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wakipita katika moja ya kipenyo cha Chiwindi Wilayani Nyasa kinachopakana na nchi jirani ya Msumbiji  karibu na mpaka rasmi wa Mbababay  unaotenganisha nchi ya Tanzania na Msumbiji. 
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Christina S. Mndeme akitoa maelekezo  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa baada ya kumaliza ziara ya mipakani

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni