Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

15 Mei 2020

NMB Yaikabidhi Idara ya Uhamiaji Vifaa vya Kujikinga na Virusi vya Corona (COVID 19)


Idara ya Uhamiaji nchini imepokea vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Ugonjwa wa Covid 19 unaosababishwa na virusi vya Corona, kutoka katika Benki ya NMB, ikiwa ni moja ya jitihada za kuunga mkono serikali katika kupambana na kudhibiti maambukizi ya ugojwa huo ulioeneo duniani kote.

Mapema leo hii akipokea Vifaa hivyo katika Ofisi ndogo ya Makao makuu ya Uhamiaji Tanzania iliyopo Kurasini Jijini Dar es salaam Kamishna wa Uhamiaji Divisheni ya Pasipoti na Uraia Gerald Kihinga ameishukuru Benki hiyo kwa kutoa vifaa hivyo na kuahidi kuvitumia ipasavyo ili viweze kuwasaidia wananchi wanaokuja kupata huduma mbali mbali za kiuhamiaji sanjari na Maofisa, Askari na watumishi wa Idara  ili kuweza kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.


“Kama mnavyojua maelekezo ya serikali ni kwamba tunapoendelea kutoa huduma zetu ni lazima kuzingatia maelekezo ya wizara ya afya na wataalamu wake kwa kuvaa vifaa kinga, kunawa mikono, na kupeana nafasi baina ya mtu na mtu na hilo tunalizingatia sana ili kuhakikisha Maofisa Askari na Wananchi kwa ujumla wanakuwa salama wakati wote” alisema

Aidha Kamishna Kihinga amewataka watanzania kutokua na hofu wanapoingia katika ofisi yoyote ya uhamiaji kupata huduma kwani tahadhari zote za kuwalinda na kujikinga na maambukizi zinachukuliwa kwa umuhimu wa hali ya juu sana.

Kwa Upande wake Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es salaam Bw. Badru Idd akikabidhi vifaa hivyo ameishukuru Idara ya Uhamiaji kwa kufanya kazi Kwa ukaribu na NMB lakini pia amewataka watanzania kutokua na hofu bali wachukue tahadhari zote Kwa kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na barakoa, vitakasa mikono, vifaa vya kuhifadhia vitakasa mikono na vifaa vya kuhifadhia sabuni.


HABARI PICHA NA MATUKIO
Kamishna wa Uhamiaji Divisheni ya Pasipoti na Uraia Gerald Kihinga (Kulia) akipokea Moja ya vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Ugonjwa wa Covid 19 kutoka kwa Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es salaam Bw. Badru Idd 
Kamishna wa Uhamiaji Divisheni ya Pasipoti na Uraia Gerald Kihinga Akitoa salamu za shukrani kutoka Uhamiaji mara baada ya kupokea vifaa
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es salaam Bw. Badru Idd akitoa malezo mafupi ya vifaa walivyotoa kwa Uhamiaji mapema leo hii katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini Jijini Dar es salaam



Viongozi Waandamizi na Maofisa mbali mbali wa Uhamiaji wakisikiliza kwa makini maelezo ya vifaa vilivyotolewa na NMB (Wengine ni Watumishi wa benki ya NMB) 

 



Picha ya Pmoja Baina ya watumishi wa Benki ya NMB Na Viongozi Kutoka Uhamiaji (Picha zote na Kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Makao Makuu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni