Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

10 Januari 2022

*Waziri Mpya na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Wapokelewa Wizarani kwa Bashasha.*

 Na. Konstebo Amani Mbwaga, Dodoma

Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) na Naibu Waziri Mpya Mhe. Jumanne A. Sagini (Mb) wamewasili leo katika Ofisi ya Makao Makuu ya Wizara iliyopo Mtumba Jijini Dodoma na kupokelewa na watumishi wa Wizara hiyo na baadhi ya watendaji kutoka katika taasisi mbalimbali zilizopo chini ya Wizara hiyo ikiwemo Jeshi la Uhamiaji ambalo liliwakilishwa na Kamishna wa Uhamiaji Fedha na Utawala Kamishna Hamza Shaban.

Akiongea na Watumishi Wizarani hapo Mhe. Masauni alisema amefurahi kurudi kwenye familia yake kwani miaka ya nyuma aliwahi kuwa Naibu Waziri Wizarani hapo na hivyo amewataka watumishi hao kushirikiana ili kumsaidia Mhe. Rais katika kutekeleza adhma yake ya kuwatumikia watanzania na kuwaletea maendeleo.

Kabla ya uteuzi huo Mhe. Masauni alikuwa Naibu Waziri Wizara ya Fedha na Mipango.

Kwa upande wake Naibu Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini amewashukuru watumishi wa wizara kwa mapokezi mazuri na amewaahidi kutumia uzoefu wake wa utumishi wa umma kwa muda miaka zaidi ya 30 kuleta mabadiliko chanya wizarani hapo kwa faida ya vizazi vya sasa na baadae.

Mhe. Sagini pia ni Mbunge wa Jimbo la Butiama lililoko Mkoani Mara.

Viongozi hao waliwasili katika ofisi za Wizara mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan jana tarehe 10 Januari 2022 Ikulu Chamwino Jijini Dodoma.

Aidha viongozi wengine walioteuliwa kubaki katika nafasi zao katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ni Katibu Mkuu Ndugu. Christopher Kadio na Naibu Katibu Mkuu Ndugu. Ramadhani Kailima.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inaundwa na taasisi mbalimbali ikiwemo Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, Jeshi la Uhamiaji, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA huku ikiwa na Majukumu ya Kulinda Usalama wa Raia na Mali zao , Kuhifadhi na Kurekebisha Wafungwa, Kudhibiti Uingiaji na Utokaji wa Raia na Wageni, Kutoa huduma za Zimamoto na Uokoaji, Kuwahudumia Wakimbizi, na Kuandaa Vitambulisho vya Taifa.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) akifurahia jambo na Naibu Waziri Mpya Mhe. Jumanne A. Sagini (Mb) baada ya kuwasili jana katika Ofisi ya Makao Makuu ya Wizara iliyopo Mtumba Jijini Dodoma na kupokelewa na watumishi wa Wizara hiyo. 

Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Bw. Christopher Kadio alipowasili katika ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma

Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Bw. Ramadhani Kailima alipowasili katika ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma

Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) akisalimiana na Kamishna wa Uhamiaji Fedha na Utawala Hamza Shabani alipowasili katika ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma

Naibu Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne A. Sagini (Mb) jana akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Ramadhani Kailima katika Ofisi ya Makao Makuu ya Wizara iliyopo Mtumba Jijini Dodoma


Naibu Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne A. Sagini (Mb) jana akisalimiana na Kamishna wa Uhamiaji Fedha na Utawala Hamza Shabani katika Ofisi ya Makao Makuu ya Wizara iliyopo Mtumba Jijini Dodoma








Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) akisalimiana na Watumishi mbalimbali wa Wizara alipowasili katika ofisi za Wizara Mtumba Jijini Dodoma





Kamishna wa Uhamiaji Fedha na Utawala Hamza Shabani












Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) akiongea na watumishi wa Wizara na wawakilishi kutoka katika Taasisi zilizochini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (Hawapo Pichani)





Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakiwa katika Picha ya Pamoja

Picha ya Pamoja 



Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) akiwa na Naibu Waziri Mpya Mhe. Jumanne A. Sagini (Mb) baada ya kuwasili jana katika Ofisi ya Makao Makuu ya Wizara iliyopo Mtumba Jijini Dodoma.


Waziri Mpya wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Y. Masauni (Mb) akiwa na Mkewe baada ya kuwasili jana katika Ofisi ya Makao Makuu ya Wizara iliyopo Mtumba Jijini Dodoma.



















(Picha zote na Konstebo Amani Mbwaga)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni