Matangazo
08 Septemba 2019
05 Septemba 2019
31 Agosti 2019
IDARA YA UHAMIAJI YATAKIWA KUJIIMARISHA KATIKA KUVUTIA WAWEKEZAJI NCHINI
Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi, Mhe Kangi Lugola ameitaka Idara ya Uhamiaji kuimarisha uwekezaji nchini.
Wito huo umetolewa leo Mjini Moshi wakati akifungua Mkutano wa Maafisa Uhamiaji
Waandamizi unao
lenga kujadili na kutathmini utendaji kazi wa Idara ya Uhamiaji.
Akizungumza na Maafisa hao, Waziri Lugola
amesisitiza kuwa nchi yetu inazo fursa nyingi za kiuchumi na Utalii hivyo
kuwavutia wageni na wawekezaji wengi kuiingia na kuwekeza nchini.
“Katika utendaji kazi
wake,Idara ya uhamiaji ndio kioo/taswira ya nchi yetu hivyo tufanye kazi kwa weledi na kuweka mazingira
bora ya uwekezaji na kuwahudumia wageni kwa ukarimu, lugha za staha na msiwe
kikwazo cha uwekezaji na utalii nchini”
alisema Waziri Lugola.
Aidha, Waziri Lugola
amemuagiza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji kusimamia kikamilifu Ukusanyaji wa
Maduhuli ya Serikali na kudhibiti mianya inayopelekea upotevu wa maduhuli.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa
wa Kilimanjro, Mhe. Anna Mghwira ametoa wito kwa Idara ya Uhamiaji kushiriki
kikamilifu katika zoezi la uandikishaji na utoaji wa Vitambulisho vya Taifa
(NIDA).
“Mkoa wa Kilimanjaro una
idadi kubwa ya Wahamiaji haramu kutokana na jiografia yake pamoja na kuwepo kwa
fursa mbalimbali za uwekezaji na utalii. Ili kukabiliana na changamoto hii,
Idara iimarishe udhibiti wa mipaka ya nchi yetu ikiwa ni sambamba na kuwatambua
Watanzania na raia wa kigeni wanaoishi na kufanya kazi nchini”, aliongeza Mhe.
Mghwira.
Mhe. Mghwira ameitaka pia
Idara ya Uhamiaji kujenga mahusiano na Wananchi ili kupata taarifa za haraka na
sahihi kutoka kwa wananchi hao.
“Nitoe wito kwa Idara ya
Uhamiaji kubuni mbinu na mikakati kwa Maafisa wake kushuka chini kwa Wananchi
ili kuwa karibu zaidi na jamii na Watanzania kwa ujumla. Kwa kufanya hivyo
Wananchi watajua haki zao ikiwa pamoja na kufahamu vielelezo vinavyotakiwa
katika kupata huduma za Idara ikiwamo Pasipoti sanjali na kutoa taarifa juu ya
uwepo wa wahamiaji haramu katika maeneo yao amesisitiza Mhe. Mghwira.
Awali akimkaribisha Mhe.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi katika Mkutano huo, Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala amesema kuwa Idara imezindua mpango mkakati
wa kudhibiti Uhamiaji nchini. Mpango huo unalenga kuwatambua na kuwaorodhesha
wahamiaji wote nchini na zoezi hilo litafanyika nchi nzima kwa kuanzia Mkoa wa
Dar es Salaam.
Katika utekelezaji wake,
mpango huo utahusisha Viongozi wa Serikali za Mitaa au Vijiji (MEO/VEO),
Maafisa Watendaji wa Kata (WEO) na kuratibiwa na Idara ya Uhamiaji. Kupitia
Mpango huo Idara itaimarisha udhibiti na usimamizi wa mipaka yetu, kuimarisha
ulinzi na Usalama na pia kulipatia ufumbuzi suala la Wahamiaji Walowezi.
30 Agosti 2019
WAZIRI LUGOLA KUFUNGUA MKUTANO WA MAAFISA UHAMIAJI WAANDAMIZI
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Kangi Lugola kesho Jumamosi tarehe 31
Agosti anatarajiwa kufungua mkutano wa Maafisa Uhamiaji Waandamizi kutoka mikoa
ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Akitoa
taarifa hiyo mjini Moshi leo, Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Mrakibu Mwandamizi
Alhaji Ally Mtanda amesema kuwa mkutano huo wa siku mbili chini ya Uenyekiti wa
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala utafanyika katika Chuo cha
Kikanda cha Uhamiaji (TRITA) mjini Moshi una lenga kujadili na kutathmini utendaji
kazi wa idara pamoja na kukumbushana masuala mbalimbali hususan Sheria, Kanuni
na Taratibu ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na raia wa kigeni.
“Mkutano
huu utahudhuriwa na Makamishna wa Uhamiaji, Maafisa Uhamiaji Mikoa yote Tanzania
na Zanzibar, Wakuu wa Vitengo pamoja na Wafawidhi wa Vituo vya Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid
Amani Karume (AAKIA), Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA),
Namanga, Tunduma na Bandari ya Zanzibar.” Aliongeza Alhaji Mtanda.
14 Mei 2019
IDARA YA UHAMIAJI YAIKABIDHI SUMAJKT MRADI WA UJENZI WA JENGO LA MAKAO MAKUU DODOMA
Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna P. Makakala jana alikabidhi Mradi wa Ujenzi wa jengo la ghorofa nane
ambalo litakuwa Makao Makuu mpya ya Uhamiaji
eneo la NCC, Kitalu na 18 na 19, jijini Dodoma kwa wakandarasi wa SUMAJKT.
Kamishna
Jenerali alisema " tunaijua sifa ya
SUMAJKT kupitia mifano mbalimbali ya
majengo bora ambayo wameyakamilisha kwa wakati, na kwa ukweli huu nina
imani kubwa nao ya kwamba jengo letu litajengwa kwa ustadi wa hali ya juu na
hivyo kuwa ni moja ya majengo ya kisasa yanayovutia hapa jijini Dodoma".
Kwa upande mwingine tukio hili lilihudhuliwa
na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja
Jenerali Martin Busungu na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT, Kanali Mabele ambaye
aliahidi kuwa shirika lake litajenga jengo ambalo litakuwa ni kioo cha ubora wa
kazi zao na kwamba watu hawata hitaji kwenda jijini Dar es Salaam kuona mifano
ya kazi zao bali hapa Dodoma tu.
Aidha,
tukio hili lilishuhudiwaa na Mkuu wa Timu ya washauri
waelekezi wa Mradi, Dkt. Msanifu Majenzi, Isabela Mtani kutoka Chuo Kikuu cha
Ardhi, Dar es Salaam ambaye alisema kuwa
makabidhiano ya Mradi huo wa Ujenzi kati ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni mmiliki
na SUMAJKT ambayo ni Mkandarasi yatafuatiwa na shughuli nyingi ambazo
zimepangwa kwenda kwa haraka sana na bila kuathili ubora wa kazi yenyewe na
jengo linalojengwa.
Mradi wa
jengo hilo ambalo litakuwa kubwa kuliko lile la Kurasini, Dar es Salaam na
ambalo lilikuwa Makao Makuu ya zamani linatarajiwa kukamilika ndani ya kipindi
cha miezi 18, na kuiwezesha Idara ya Uhamiaji kuanza kutumia jengo bora lenye
hadhi ya kimataifa jijini Dodoma.
09 Mei 2019
UHAMIAJI YATOA ONYO KALI KWA MAWAKALA (VISHOKA) WANAOTUMIA VIBANDA VYA WAJASIRIAMALI VILIVYOPO MKABALA NA OFISI YA UHAMIAJI MAKAO MAKUU KUWATAPELI WANANCHI.
Kaimu
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Hanelore Manyanga amekutana
na wafanya biashara na wajasiriamali wanaofanya biashara katika mtaa wa
Loliondo, Kurasini - Jijini Dar es salaam. Mtaa huo upo Mkabala na Ofisi za
Uhamiaji Makao Makuu na kuna shughuli mbalimbali za biashara ikiwamo Mamalishe,
Mawakili, Wapiga picha (Passport size)
pamoja na watoa huduma za Stationaries.
Kamishna Manyanga amewataka
wafanya biashara hao kuisaidia Idara ya Uhamiaji kupiga vita mawakala wa huduma
za Uhamiaji (Vishoka ambao wanawatapeli wananchi wanaohitaji huduma za Uhamiaji
katika maeneo hayo.
“Kumekuwepo
na wimbi la Matapeli wanaojifanya kuwa Maafisa Uhamiaji wanawatapeli Wananchi
kwa kuchukua pesa zao na kuwaahidi kuwasaidia kupata huduma za Uhamiaji ikiwa
ni pamoja na Pasipoti, Viza, na Hati za Ukaazi kwa haraka. Kupitia kikao hiki nawaagiza
kuwa mfanye biashara kwa mujibu wa matakwa ya leseni zenu kama inatokea kuna
mtu ambaye siyo mhusika au anatumia vibanda vyenu kuwatapeli wananchi, tafadhali
toeni taarifa Uhamiaji” alisema
Kamishna Hanelore Manyanga
Aidha, Kamishna Manyanga aliongeza
kuwa Idara ya Uhamiaji imedhamiria kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya
wale wote wanaojifanya Maafisa Uhamiaji na kuwatapeli Wananchi.
Wakitoa maoni yao katika kikao hicho baadhi ya
wajasiriamali hao wametoa maoni yao na kuonesha kuchukizwa na vitendo hivyo
ambavyo vinafanywa na watu ambao siyo waadilifu na kuchafua taswira nzuri ya
Idara ya Uhamiaji na biashara zao kwa ujumla.
“Ni
jambo jema kualikwa hapa kujadili suala hili, hata sisi tumekuwa tukichukizwa
na hawa watu lakini tunashindwa kutoa taarifa kwani hatujui tumwambie nani,
unakuta mtu anakuja pale mgahawani na mtu wanasaidiana kujaza fomu za Uhamiaji na
baadae wanaondoka. Kupitia kikao hiki sasa tutakuwa tunatoa taarifa Uhamiaji
lakini tunaomba tukitoa taarifa hizo zifanyiwe kazi na pia taarifa hizo ziwe
siri” alisema Bi. Praise
Kupitia Kikao hicho wafanya
biashara hao kwa pamoja wameahidi kushirikiana na Idara ya Uhamiaji na
kuwafichua Mawakala/Vishoka wanaotumia Ofisi za mawakili, stationeries na
migahawa kufanyia shughuli za Uhamiaji ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa
yeyote atakayejihushisha na kazi za Uhamiaji katika maeneo yao ikiwa ni pamoja
kufikishwa Mahakamani.
Kwa upande wake Kamishna wa
Uhamiaji, Uraia na Pasipoti Gerald J. Kihinga, ametoa wito kwa Wananchi kuwa
hakuna Uwakala katika huduma zinazotolewa na Idara ya Uhamiaji. Hivyo mtu
anayeomba Pasipoti ya Tanzania au Vibali vya Ukaazi anatakiwa awasilishe maombi
yake kupitia tofuti ya Idara ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni www.immigration.go.tz
Kikao hicho kilihudhuriwa pia
na Kamishna wa Uhamiaji, Uraia na Pasipoti Gerald J.
Kihinga, Kaimu Kamishna wa Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka, Naibu Kamishna
wa Uhamiaji, Paul Eranga pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Uratibu, Mrakibu
Mwandamizi wa Uhamiaji Peter G. Mbaku.
| Bi. Praise akichangia hoja katika kikao hicho. |
| Bw. Mulokozi ambaye ni mjasiriamali katika moja ya vibanda vilivyo mkabala na Ofisi ya Uhamiaji akieleza utayari wake katika kukabiliana na tatizo la vishoka wakati wa kikao hicho |
| Kaimu Kamishna wa Usimaizi na Udhibiti wa Mipaka, naibu Kamishna Paul Eranga akiongea wakati wa kikao hicho |
| Kaimu Kamishna wa Uhamiaji, Kamishna Hannelore Manyanga akiongea wakati wa kikao hicho |
| Kamishna wa Uraia na Pasipoti, Kamishna Gerald Kihinga akiongea wakati wa kikao hicho |
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)



