Matangazo
16 Aprili 2019
14 Aprili 2019
10 Aprili 2019
07 Aprili 2019
06 Aprili 2019
TANZANIA, ETHIOPIA NA KENYA ZAKUTANA KUTAFUTA SULUHISHO LA KUTATUA TATIZO LA WAHAMIAJI HARAMU NA KUIMARISHA USHIRIKIANO MIPAKANI
Tanzania imekuwa mwenyeji wa
Mkutano wa Ngazi ya juu wa Kikanda
uliofanyika katika Hotel ya Serena, Dar es Salaam kuanzia tarehe 02-04 April mwaka
huu.
Mkutano
huo ulihudhuriwa na viongozi waandamizi kutoka nchi za Tanzania, Kenya, Ethiopia,
Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) na Wadau wa Maendeleo (Development Partners)
ambao ni Balozi za Uingereza, Marekani, Ujerumani, Norway, Ubelgiji, EU, UN-RCO,
na ICRC na kufunguliwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Alphaxad
Lugola ulilenga kutafuta njia ya namna
ya kukabiliana na ongezeko la wahamiaji haramu, wanaoingia kinyume cha sheria
hapa nchini kupitia njia ya Kusini (Southern route).
Mkutano
huo ulitanguliwa na mkutano wa Wataalamu
wa masuala ya uhamiaji kutoka nchi za Tanzania, Ethiopia na Kenya chini ya
Uenyekiti wa Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala.
Pamoja
na mambo mengine nchi hizo zimeweka mikakati ya pamoja katika kushughulikia changamoto
ya biashara haramu ya binadamu (Human Trafficking
& Smuggling) na usafirishaji kimagendo wa binadamu (Human Smuggling), kuangalia
namna bora ya kubadilishana taarifa za Wasafirishaji (Traffickers &
Smugglers) na mikakati ya kuwaondosha nchini wahamiaji haramu na kuhakikisha
hawarejei tena nchini bila kufuata taratibu.
“Ni
mkutano wenye nia njema kwa nchi yetu, kwani hapa tumekutana ili kuweka
mikakati namna ya kudhibiti mfumo mzima wa biashara haramu ya binadamu na usafirishaji
magendo ya binadamu kutoka pembe ya Afrika kupitia njia ya Kusini ambapo
Tanzania ni sehemu ya hiyo njia. Majadiliano yameenda vyema na tutegemee
matokeo mazuri. Kila nchi mwalikwa imeahidi kufanya juhudi katika kudhibiti
tatizo hili”
Alieleza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala.
Tanzania
imekuwa ni njia ya Usafirishaji wa Magendo ya Binadamu kuelekea kusini mwa
Afrika ambapo Idara ya Uhamiaji nchini kwa kipindi cha mwezi Januari hadi
Disemba 2018 ilifanikiwa kuwamata na kuwachukulia hatua mbalimbali jumla ya wahamiaji
haramu 1024 kutoka pembe ya Afrika wengi
wao wakiwa raia wa Ethiopia.
Hatua
mbalimbali za kudhibiti tatizo hili zimeendelea kuchukuliwa, tayari jumla ya wahamiaji
haramu 583 kutoka Ethiopia waliomaliza adhabu ya kutumikia vifungo katika
magereza mbalimbali nchini walirejeshwa nchini kwao katika kipindi cha mwaka
jana.
Aidha
katika kipindi hicho, vyombo vya usafiri 10 vilitaifishwa na Serikali baada ya
kutiwa hatiani kwa kosa la kusafirisha wahamiaji haramu kinyume cha Sheria za Uhamiaji.
“Tunaishia
kuwakamata dereva wa Fuso anaepakia wahamiaji haramu, Tunataka madalali wenyewe
wasakwe wakamatwe, Kwahiyo Kamishna Jenerali wa Uhamiaji ndani ya mwezi mmoja
angalau basi kwa uchache uje na orodha ya hawa madalali wawili watatu hata kama
ntaambiwa kwamba wako nchi nyingine ili
tuweze kutumia sheria zilizopo kuweza kuwakamata na kuwarejesha nchini ili
kumaliza huo mtandao” Aliagiza
Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, Mheshimiwa Kangi Lugola.
Mkutano
huu unategemea kuleta matokea chanya kwa Idara ya Uhamiaji katika suala zima la
udhibiti wa wahamiaji haramu kwani ni wa kwanza kufanyika na kuwashirikisha
wadau kutoka nchi za pembe ya Afrika ambako ndiko wahamiajii haramu wengi
wanaokamatwa nchini hutokea pamoja na Washirika wa Maendeleo.
28 Machi 2019
Pasipoti Mpya ya Tanzania ya Kilektroniki yatunikiwa Tuzo ya Ubora
![]() |
| Kamishna wa Uhamiaji (Pasipoti na Uraia) Gerald Kihinga (katikati) akiwa na Tuzo hio |
Pasipoti Mpya ya
Tanzania ya Kielektroni imetunikiwa Tuzo ya Pasipoti Bora katika Ukanda wa Ulaya,
Mashariki ya Kati na Afrika (Europe, Middle East and Africa - EMEA) kwa kukidhi
Viwango vya Ubora wa Kimataifa vinavyopendekezwa na Shirika la la Umoja wa
Mataifa linalosimamia Usafiri wa Anga (International Civil Aviation
Organisation - ICAO) kwa Mwaka 2019 katika Sherehe zilizofanyika Kisiwa cha
Malta siku ya Jumanne tarehe 26 Machi 2019.
Tuzo ambazo
huaandaliwa na kutolewa na Taasisi ya RECONNAISSANCE ambayo huzingatia ubora na
usalama wa Uchapishaji wa Nyaraka za Kielektroniki kama vile Vitambulisho vya Taifa,
fedha za noti na Pasipoti. Vipengele vinavyozingatiwa katika Tuzo hizi ni
pamoja na Usalama wa nyaraka, Usanifu, tekinolojia, na Utambulisho wa nchi.
Katika kipengele cha
utambulisho wa nchi yetu (National Identity), Pasipoti hii imesanifiwa kwa
kuzingatia utamaduni wa Kitanzania na maliasili tulizonazo ambazo ni fahari ya
nchi yetu. Michoro iliyopo katika Pasipoti hiyo ni pamoja Wanyama, majengo ya
kihistoria, Matukio ya Kitaifa na Nukuu za Hamasa za Hayati baba wa Taifa Mwalimu
Julius Nyerere.
Katika kipengele cha Usalama,
Pasipoti hii ina kifaa maalum chenye uwezo wa kutunza taarifa za mmiliki wa
pasipoti “Micro Chip” na hivyo kufanya suala la utunzaji wa usalama wa pasipoti
hizi kuwa wa hali ya juu zaidi. Pasipoti hii ina uwezo wa kutunza kumbukumbu za
kibailojia (Biometric features). Pia
pasipoti hii ni ngumu kughushiwa na wahalifu au watu wanaojaribu kuficha
utambulisho wao kwa kutumia pasipoti zisizo zao.
Ikumbukwe kuwa,
Utekelezaji wa Mradi huu umefanyika kwa muda mfupi takribani miezi minne tangu
kusainiwa kwa mkataba na ukihusisha utoaji wa Pasipoti za aina tatu (Ordinary,
Service & Diplomatic)
Tuzo hiyo ilipokelewa na
Kamishna wa Uhamiaji (Pasipoti na Uraia) Gerald Kihinga kwa niaba ya Serikali
ya Tanzania na Idara ya Uhamiaji.
24 Machi 2019
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)





