Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

28 Machi 2019

Pasipoti Mpya ya Tanzania ya Kilektroniki yatunikiwa Tuzo ya Ubora

Kamishna wa Uhamiaji (Pasipoti na Uraia) Gerald Kihinga (katikati) akiwa na Tuzo hio


Pasipoti Mpya ya Tanzania ya Kielektroni imetunikiwa Tuzo ya Pasipoti Bora katika Ukanda wa Ulaya, Mashariki ya Kati na Afrika (Europe, Middle East and Africa - EMEA) kwa kukidhi Viwango vya Ubora wa Kimataifa vinavyopendekezwa na Shirika la la Umoja wa Mataifa linalosimamia Usafiri wa Anga (International Civil Aviation Organisation - ICAO) kwa Mwaka 2019 katika Sherehe zilizofanyika Kisiwa cha Malta siku ya Jumanne tarehe 26 Machi 2019.
Tuzo ambazo huaandaliwa na kutolewa na Taasisi ya RECONNAISSANCE ambayo huzingatia ubora na usalama wa Uchapishaji wa Nyaraka za Kielektroniki kama vile Vitambulisho vya Taifa, fedha za noti na Pasipoti. Vipengele vinavyozingatiwa katika Tuzo hizi ni pamoja na Usalama wa nyaraka, Usanifu, tekinolojia, na Utambulisho wa nchi.
Katika kipengele cha utambulisho wa nchi yetu (National Identity), Pasipoti hii imesanifiwa kwa kuzingatia utamaduni wa Kitanzania na maliasili tulizonazo ambazo ni fahari ya nchi yetu. Michoro iliyopo katika Pasipoti hiyo ni pamoja Wanyama, majengo ya kihistoria, Matukio ya Kitaifa na Nukuu za Hamasa za Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Katika kipengele cha Usalama, Pasipoti hii ina kifaa maalum chenye uwezo wa kutunza taarifa za mmiliki wa pasipoti “Micro Chip” na hivyo kufanya suala la utunzaji wa usalama wa pasipoti hizi kuwa wa hali ya juu zaidi. Pasipoti hii ina uwezo wa kutunza kumbukumbu za kibailojia (Biometric features). Pia pasipoti hii ni ngumu kughushiwa na wahalifu au watu wanaojaribu kuficha utambulisho wao kwa kutumia pasipoti zisizo zao.
Ikumbukwe kuwa, Utekelezaji wa Mradi huu umefanyika kwa muda mfupi takribani miezi minne tangu kusainiwa kwa mkataba na ukihusisha utoaji wa Pasipoti za aina tatu (Ordinary, Service & Diplomatic)
Tuzo hiyo ilipokelewa na Kamishna wa Uhamiaji (Pasipoti na Uraia) Gerald Kihinga kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Idara ya Uhamiaji. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni