Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

18 Julai 2018

Kamishna Jenerali awahakikishia raia wa Msumbiji na Tanzania usalama juu ya maisha yao

WAKIMBIZI KUTOKA MSUMBIJI WAHAKIKISHIWA USALAMA WAO.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Dakta ANNA MAKAKALA amewahakikishia raia kutoka nchini Msumbiji ambao wamewasili katika kijiji cha KIVAVA wilaya ya Mtwara kwa madai ya kukimbia machafuko yaliyotokea nchini mwao watarejea kwao katika hali ya amani na usalama.

Raia hao ambao wako chini ya uangalizi wa serikali ya Tanzania tokea kuingia kwao Julai mwaka huu, walielezwa na Kamishna Jenerali Dakta MAKAKALA amesema kilichobaki hivi sasa ni kufanya mawasiliano na nchi yao ili kuona namna ya kuwarejesha. 

Akizungumza na raia hao kwa lengo la kuwajulia hali, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini Dakta ANNA MAKAKALA amewahakikishia kwamba watarejea nchini mwao wakiwa salama.

Hawa ni raia kutoka nchini Msumbiji ambao wameweka kambi katika kijiji cha KIVAVA wilaya ya Mtwara wakipatiwa huduma mbalimbali za kijamii na serikali ya Tanzania kwa madai ya kukimbia machafuko ambayo yametokea nchini mwao.

Tarehe kumi Julai 2018 serikali ilianza kupokea raia 544 wa kitanzania na raia 102 wa Msumbiji ambao wote hao walikuwa wanaishi nchini Msumbiji wakijishughulisha na kilimo.

SAID MANDANDA ni mmoja wa raia hao wa  Msumbiji kutoka kitongoji cha Mapondo kijiji cha Ujamaa Kisungule wilaya ya Palma na hapa anamueleza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Dakta ANNA MAKAKALA ambaye amewasili katika kijiji cha KIVAVA kuzungumza na raia hao.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni