Matangazo

📢 IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA — KARIBU KWENYE BLOG RASMI   ✦   📰 UHAMIAJI HABARI BLOGU — TUNAKULETEA MATUKIO KILA SIKU   ✦   📲 FUATA IDARA YETU KATIKA MITANDAO YA KIJAMII   ✦   ✉️ WASILIANA NASI: info@immigration.go.tz   ✦   ☎️ +255-22-2850575/6

23 Februari 2019

MICHEZO YA MAJESHI YAFUNGULIWA RASMI UWANJA WA UHURU JIJINI DAR ES SALAAM.

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mheshimiwa Balozi Seif Iddi leo tarehe 23 Februari 2019, amefungua Mashindano ya Majeshi ya Tanzania, Uwanja wa Uhuru, Temeke jijini Dar es salaam, ambapo Timu za soka (wanaume) JKT na Ngome ndizo zilizofungua dimba la michezo hii.

Mashindano haya yaliyoanza leo yanatarajiwa kufikia tamati tarehe 8 Machi 2019, yanahusisha Vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama nchini ambavyo ni JWTZ, JKT, Polisi, Magereza, Uhamiaji, Zimamoto na Vikosi Maalumu kutoka Zanzibar.
Michezo hi itashirikisha wanamichezo wa soka (wanaume), ngumi (wanaume), Netiboli (Wanawake), Mpira wa Mikono, Wavu, Kikapu na kulenga shabaha zitashirikisha wanaume na wanawake.














Hakuna maoni:

Chapisha Maoni