Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

14 Februari 2019

RAIA 8 WA ETHIOPIA WAZIKWA MAKABURI YA MANISPAA YA JIJI LA TANGA LEO FEBRUARI 14, 2019.

Raia wanane wa Ethipoia waliofariki tarehe 22 Oktoba 2018 hatimaye wamezikwa jijini Tanga katika makaburi ya Manispaa maafuru kwa jina la 'Neema'.

Mkuu wa Wilaya ya Tanga mjini Mhe. Thobias Mwilapwa aliongoza Mazishi hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, ambapo Balozi wa Ethiopia, viongozi wa dini pamoja na wanachi wa kawaida walihudhuria.

Balozi wa Ethiopia nchini Tanzania Mhe. Yonas Yosef Sanbe ameishukuru Serikali ya Tanzania, Uongozi wa Mkoa wa Tanga, Idara ya Uhamiaji, Hospitali ya Rufaa mkoa Tanga na Taasisi za kidini mkoa wa Tanga kwa ushirikiano waliouonesha kufanikisha mazishi ya raia hao. Pia alisema kuwa kila nci inao wajibu wa kupambana na wahamiaji haramu hivyo anapongeza juhudi za serikali katika kuthibiti wahamiaji haramu nchini.

Ibada ya kuwaombea marehemu iliendeshwa na viongozi wa dini kutoka madhehebu ya kikristo na kiislamu, ambapo Kanisa la KKKT iliwakilishwa na na Mchungaji Warehema Chamshana, Kanisa la Waadventista Wasabato alikuwepo Mwinjilisti Elitumaini Mchomvu na kwa upande wa Waislamu aliyewaombea marehemu ni Maalim Juma bin Salum wa wa Msikiti wa Masjid Sayyidna Bilal Rabbah katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga

Ikumbukwe kwamba, mnamo tarehe 22 Oktoba mwaka jana, waethipoia hao waliokotwa kando ya bahari ya Hindi nje kidogo ya jiji la Tanga wakiwa wamekufa. Baada ya uchunguzi wa kina, Idara ya Uhamiaji mkoani Tanga ilibaini kuwa walikuwa raia wa Ethiopia waliokuwa wakisafirishwa kwa njia ya haramu kuelekea Afrika ya Kusini










Maoni 1 :