Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

28 Septemba 2019

NAIBU KATIBU MKUU RAMADHAN KAILIMA ATEMBELEA OFISI YA UHAMIAJI MAKAO MAKUU

Naibu Katibu Mkuu Ramadhani Kailima na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala wakifurahia jambo na wananchi ambao wapo kwenye foleni ya kusubiria huduma ya kupewa pasipoti kwa dharura.

Mkuu wa Kitengo cha Tehama Kamishna Msaidizi Mwandamizi Mohamed Awesu akimwonyesha Naibu Katibu Mkuu namna mfumo wa Tehama wa e-Immigration unavyofanya kazi nchi nzima


Naibu Katibu Mkuu Ramadhani Kailima akiangalia pasipoti ya kieletroniki baada ya kuchapishwa alipotembelea chumba cha Passport Printing, Uhaimiaji Makao Makuu.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ramadhani Kailima akingalia jinsi pasipoti inavyokaguliwa katika mfumo kwenye hatua ya mwisho kabla ya kutolewa ili itumike

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Ramadhani Kailima
ametembelea Ofisi ya Uhamiaji Makao Makuu Dar es Salaam na kujionea namna  Idara hiyo ilivyojipanga kuwahudumia Wananchi.


 Akiwa Ofisini hapo, Naibu Katibu Mkuu huyo alipata fursa ya kukagua Mfumo wa utoaji wa huduma ya Pasipoti.


 Maeneo aliyotembelea na kukagua ni Kaunta ya kupokelea maombi, Chumba maalum cha kuchukulia alama za vidole kielektroniki, Ofisi ya Uhakiki na Udhinishaji wa maombi hayo pamoja na Ofisi ya Uchapishaji wa Pasipoti (Passports' Printing Room).
 Naibu Katibu Mkuu huyo pia amekagua Kitengo cha Utoaji wa Pasipoti kwa haraka/dharura kwa Wananchi wenye mahitaji maalum.


 Kabla ya kuhitimisha Ziara yake, Naibu Katibu Mkuu Kailima alipata fursa ya kuzungumza na Wananchi na raia wa kigeni walifika Ofisini hapo kwa ajili ya kupatiwa huduma mbalimbali za kiuhamiaji.


 Aidha, Naibu Katibu Mkuu Kailima amemuagiza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala kuanzisha utoaji wa huduma za Pasipoti kwa haraka (express).
 "Nimelezwa kuwa kwa sasa Waombaji wa Pasipoti wanapatiwa kwa muda siku  ..., Hivyo  anzisheni Mfumo wa utoaji wa Pasipoti kwa haraka (express) na Wananchi watakao hitaji huduma hiyo wachangie kiasi kidogo cha fedha na kupatiwa Pasipoti zao kwa muda wa siku moja", alizungumza Kailima.


 Aliongeza kuwa wapo baadhi ya Wananchi hawapendi kutumia muda wao mwingi kwenye foleni wakati wanaweza kulipia kiasi kidogo cha fedha ili kupata huduma kwa haraka.
  Kwa upande wake Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala
alimwahidi Naibu Katibu Mkuu huyo kutekeleza maelekezo aliyoyatoa katika ziara hiyo.
 Dkt. Makakala ameongeza kuwa Idara ya Uhamiaji imejiimarisha vyema kutekeleza Mradi wa Uhamiaji Mtandao kwa lengo la kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi na wageni.
 Kupitia Mfumo huo, Jumla ya Pasipoti 187,787 na hati za dharura za safari (Emergency Traveling Documents - ETDs) 255,534 zimetolewa kwa Watanzania.


 Dkt. Makakala ameongeza kuwa Idara ya Uhamiaji inatekeleza vyema dhana kuimarisha sekta za Utalii na Uwekezaji Nchini. Kupitia Mfumo huu, Idara imetoa Vibali vya Ukaazi 6,848 kwa Wageni waliongia na kuishi Nchini kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo Uwekezaji.
  Pia Idara ya Uhamiaji imetoa viza 152,377 kwa Wageni walioingia nchini kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo Utalii na Matembezi.


 Mfumo wa Uhamiaji Mtandao unaohusisha Utoaji wa huduma za kielektroniki za Pasipoti, Viza, Vibali vya Ukaazi pamoja na Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka umezinduliwa mnao Januari 31, 2018 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni