Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

05 Oktoba 2019

“FANYENI KAZI KWA WELEDI NA KUZINGATIA SHERIA”, DKT. MAKAKALA


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala ametoa rai hiyo alipokuwa akizungumza na Watumishi wa Idara ya Uhamiaji katika Mkoa wa Mbeya.

Akizungumza na Watumishi hao, Kamishna Jenerali amewasihi kujiepusha na vitendo vya rushwa na kufanya kazi kwa weledi na bidiii ili kwenda sambamba na kasi ya serikali ya Awamu ya Tano katika kuwaletea wananchi wake maendeleo na kukuza uchumi wa nchi yetu.

“Idara ya Uhamiaji ina jukumu kubwa la kukuza sekta za Utalii na Uwekezaji katika nchi yetu hivyo tunatakiwa kuwahudumia wageni wanaoingia na kuishi nchini bila vikwazo vinavyoweza kurudisha nyuma ustawi wa sekta hizo” amesitiza Dkt. Makakala.

Kwa upande wake Afisa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya, Naibu Kamishna wa Uhamiaji Shaaban Omari ameeleza kuwa Idara inaendelea na mapambano dhidi ya Wahamiaji kwa kuwashirikisha Viongozi wa Serikali za Mitaa na Kata.

Viongozi hao Kata na Vijiji wanapatiwa Elimu ya Uhamiaji ili kuwajengea uelewa katika masuala ya Kiuhamiaji ikiwa ni maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kutekeleza Mpango Mkakati wa Mapambano dhidi ya Wahamiaji haramu (Pekenyua Fukunyua) unaondelea nchi nzima kwa sasa.

Akiwa katika ziara hiyo Mkoani Mbeya, Dkt. Makakala ametembelea na kukagua Ofisi za Uhamiaji katika Vituo vya Uwanja wa Ndege wa Songwe pamoja na Mpaka wa Kasumulu.

Kesho Jumamosi Oktoba 5, 2019, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji atahudhuria Uzinduzi wa Kituo cha pamoja cha utoaji huduma za mpakani (OSBP) katika Mpaka wa Tunduma Mkoani Songwe ambapo mgeni rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akisalimiana na Maafisa Uhamiaji Mkoa wa Mbeya mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Uhamiaji Mkoa huo siku ya Alhamisi tarehe 04 Oktoba 2019 katika ziara ya kikazi mkoani humo.


Kaimu Mfawidhi wa kituo cha Uhamiaji Kasumulo akimuonesha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji eneo litakalojengwa kityoo cha Mpaka wa Pamoja (OSBP).


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akiongea na raia wa DRC Bwana Jeane Pierre aliyekuwa akipata huduma za Uhamiaji katika mpaka wa Tunduma

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji pamoja na Kamishna wa Udhibiti na Usimamizi wa Mipaka wakiangalia ukamilishaji wa maandalizi ya ufunguzi wa kituo cha huduma za pamoja mpakani (OSBP) katika mpaka wa Tanzania na Zambia mji mdogo wa Tunduma. 

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji akisaini kitabu cha wageni katika kituo cha Uhamiaji Tunduma mkoani Songwe



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni