Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

12 Oktoba 2019

Imarisheni doria maeneo yenu” Kamishna Jenerali Dkt. Anna Makakala

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala ametoa agizo hilo alipotembelea ofisi ya Uhamiaji Mkoa Katavi ambapo pamoja na kupata taarifa ya utendaji kazi wa ofisi hiyo na kusikiliza changamoto mbalimbali, aliendelea kusisitiza watumishi wa Idara ya Uhamiaji kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na kujiepusha na vitendo vya rushwa.

“Nawataka muimarishe doria katika maeneo yenu hasa katika kipindi hiki tunapokaribia uchaguzi wa serikali za mitaa, maeneo haya yana makambi ya wakimbizi na walowezi. Hakikisheni hawajiingizi kwenye uchaguzi aidha kugombea nafasi za uongozi au kupiga kura.” Aliagiza Dkt. Makakala akiwa Namanyere.

“Mnafanya kazi nzuri sana pamoja na changamoto zilizopo, kila ofisi au kituo nInachopita maneno yangu ni yale yale nakumbusha tu kuwa kila mmoja ajitambue kuwa anatakiwa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria, kujiepusha na vitendo vya rushwa pamoja na kuzingatia motto yetu ya Nidhamu, Upendo na Mshikamano miongoni mwenu, Uwajibikaji katika utendaji kazi wenu na kukataa rushwa” alisisitiza Dkt. Makakala.


Afisa Uhamiaji Mkoa Katavi, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Vicent Haule akisoma taarifa ya Utendaji kazi mkoa Katavi mbele ya Kamishna Jenerali Dkt. Makakala.


Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya uhamiaji mkoa Katavi alipotembelea mwanzoni mwa wiki hii.



Maafisa Uhamiaji mkoa wa Katavi wakimsikiliza Kamishna Jenerali 





Kamishna Jenerali Dkt. Makakala akimsikiliza Afisa Uhamiaji Wilaya ya Nkasi Mrakibu Joseph Bulali wakati alipotembelea ofisi hiyo kuongea na watumishi
Add caption
Kamishna Jenrali akisalimiana na Maafisa wa Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa alipotembelea ofisi hiyo.


 








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni