Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

30 Oktoba 2019

Dkt. Makakala aridhishwa na kasi ya ujenzi wa Jengo la Uhamiaji Dodoma.








Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala na Kamishna wa Utawala na Fedha wa Idara hiyo, amefanya ukaguzi wa kazi ya ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji eneo la NCC, jijini Dodoma. Katika ukaguzi huu Dkt. Makakala ambaye aliambata na Kamishna wa Uhamiaji Utawala na Fedha Edward Chogero, amesifu kazi nzuri inayofanywa na wahandisi wa Kampuni ya Kizalendo ya SUMA JKT ambayo ndiyo iliyopewa zabuni ya ujenzi wa jengo hilo la ghorofa nane ambalo linalotarajiwa kuwa la kuvutia jijini humo.

Kazi ya ujenzi wa sehemu ya ardhini ya jengo hilo imekamilika na kwa sasa maandalizi ya kumwaga zege la jamvi la ghorofa ya chini yamekamilika na tayari Mshauri Mwelekezi wa Mradi huo ambaye ni Chuo Kikuu cha Ardhi ametoa idhini ya kumwaga zege ili kuruhusu hatua zaidi za ujenzi kuendelea.


Ujenzi wa Jengo hilo uinatarajiwa kukamilika ndani ya muda wa miezi 18, na kwa mujbu wa Meneja Mradi, Kanali Zablon Mahenge amesema ujenzi unakwenda kwa kasi na umakini mkubwa na kwamba kazi itakamilika kwa wakati na ubora wa hali ya juu.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni