Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

07 Oktoba 2019

“Tumejipanga kutoa huduma bora”, KAMISHNA JENERALI WA UHAMIAJI

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala akiongea na Watumishi katika Kituo cha Uhamiaji Tunduma mwishoni mwa wiki.

Kamishna wa Udhibiti na Usimamizi wa Mipaka, Kamishna wa Uhamiaji Samwel Mahirane akitoa taarifa ya utendaji kazi wa kituo cha Uhamiaji Tunduma kwa waheshimiwa Marais wa Tanzania na Zambia mra baada ya uzinduzi wa kituo cha huduma ya pamoja mpakani (OSBP) katika mpaka wa Tunduma.














Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala amewaagiza Watumishi wa Idara ya Uhamiaji kufanya kazi kwa weledi na kujiepusha na vitendo vya rushwa wakati wanapotoa huduma kwa Wananchi na raia wa kigeni.

Dkt. Makakala  ametoa wito huo ikiwa ni Utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoyatoa wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Kituo cha Pamoja cha Huduma Mpakani (One Stop Border Post - OSBP) cha Tunduma - Nakonde, tarehe Oktoba 5, 2019.

Awali Kamishna Jenerali alipokea taarifa ya utendaji kazi wa kituo hicho na amewataka kuimarisha doria maeneo ya mipakani na kushirikiana na watendaji kata na vijiji katika kuwabaini wahamiaji haramu wanaojipenyeza na kuishi katika maeneo yao.

Idara ya Uhamiaji kama mdau wa huduma mapakani hapo imeshiriki hafla uzinduzi wa Kituo hicho (Tunduma – Nakonde OSBP) uliofanywa kwa pamoja na Marais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Jamhuri ya Zambia, Mhe. Edger Lungu.  

Idara ya Uhamiaji imejipanga kutoa huduma bora na za kisasa mpakani hapo kwa kutumia mfumo wa Uhamiaji Mtandao (e-immigration) ambapo Vifaa vya kisasa vimefungwa ili kufanikisha upatikanaji wa huduma bora za Kiuhamiaji. 

Mfumo huu pia utawezesha kudhibiti mpaka huo kwa njia ya kielektroniki (e-Border Management Systems) suala ambalo litasaidia ulinzi na usalama.
Mfumo huu (e-Immigration) utatatua kero zinazosababishwa na urasimu usio wa lazima katika utoaji wa huduma za kiuhamiaji.













Hakuna maoni:

Chapisha Maoni