Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

18 Oktoba 2019

UHAMIAJI YASHIRIKI MAONYESHO YA UTALII YA “SWAHILI INTERNATIONAL TOURISM EXPO






























Katibu mkuu kiongozi  Balozi John kijazi leo amezindua maonyesho ya Utalii ya” SWAHILI INTERNATIONAL TOURISM EXPO katika viwanja vya mlimani city Dar es salaam.

Maonyesho hayo ambayo yameanza leo tarehe18 yatamalizika tarehe 20 mwezi huu yamehusisha taasisi mbalimali ikiwemo idara ya uhamiaji ambapo kama kawaida imeendelea kutoa huduma kwa wageni waalikwa pamoja na wananchi wanaohudhulia maonyesho hayo.

Kwa upande wake mgeni rasmi kwenye maonyesho hayo Balozi Kijazi amesifu maandalizi ya maonyesho hayo na kuwataka wanachi kujitokeza kujua na kujifunza mambo mbalimbali kupitia maonyesho hayo ambayo yanatarajiwa kumalizika Jumapili.

Pia balozi kijazi ameongeza  Maonyesho hayo yamesaidia sana kukuza sekta ya utalii  ikiwa ni pamoja na kuongeza  pato la taifa kupitia  sekta ya utalii nchini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni