Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

18 Novemba 2019

Mbaroni kwa kujifanya Afisa Uhamiaji




Afisa Uhamiaji ‘Feki’ Bushiri Ally Nassoro  mwenye  umri wa miaka 19 leo tarehe 18 Novemba 2019, amekamatwa na Maafisa Uhamiaji kwa tuhuma za kuwatapeli na kuwalaghai wateja wanaokuja kupata huduma za Kiuhamiaji katika ofisi ya Uhamiaji Makao Makuu Kurasini jijini Dar es salaam.

Katika mahojiano ya awali, Afisa huyo Feki  pia aligundulika  kudanganya kama Afisa Usalama wa Taifa. Kijana huyo tapeli ambaye anadai ameanza kulaghai wateja tangu mwaka 2017 bado anaendelea kushikiliwa na kuhojiwa kwa uchunguzi zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni