Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

21 Novemba 2019

MKUTANO WA WAKUU WA IDARA ZA UHAMIAJI NA KAZI WA TANZANIA NA UGANDA WAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Kamishna wa Uhamiaji (Vibali na Pasi), Mary Palmer akiongea wakati wa mkutano huo.

Kamishna Palmer akimkabidhi zawadi Mkurugenzi Mkuu wa Uraia na Masuala ya Uhamiaji wa Uganda Meja Jenerali Apollo Kassita-Gowa mara bada ya mkutano huo.


Mkurugenzi Mkuu wa Uraia na Masuala ya Uhamiaji wa Uganda Meja Jenerali Apollo Kassita-Gowa akimkabidhi zawadi Kamishna wa Uhamiaji Mary Palmer (ndc) ambaye pia ndiye aliyeongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo.







Kamishna  wa Uhamiaji Mary Palmer (ndc), anayesimamia Divisheni ya Vibali, Pasi na Visa, aliongoza ujumbe wa Idara ya Uhamiaji Tanzania katika Mkutano wa Wakuu wa Idara za Uhamiaji na Kazi za Tanzania na Uganda uliofanyika Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es salaam.

Lengo la mkutano huo ni kuzikutanisha nchi za Tanzania na  Uganda ili kujadili na kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali hususan  za kiuhamiaji zilizopo baina ya nchi hizo.

Katika Mkutano huo, Kamishna Palmer alimuwakilisha Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt Anna Peter Makakala, ambaye yuko nje ya Ofisi kwa majukumu mengine ya kikazi. Aidha, ujumbe kutoka Uganda uliongozwa na Meja Jenerali Apollo Kasiita-Gowa, ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Uraia na Masuala ya Kiuhamiaji nchini Uganda.

Akizungumza wakati wa mkutano huo Kamishna Palmer alisema, ushirikiano baina ya nchi hizo mbili ni muhimu sana katika kuimarisha udhibiti wa masuala mbalimbali ya kiuhamiaji. Pia aliongeza kusema kuwa mkutano huo utasaidia kuongeza kasi ya kuondoa vikwazo vya safari baina ya raia wa nchi za Tanzania na Uganda.

Kwa upande wake Meja Jenerali Apollo Kasiita -Gowa akieleza umuhimu wa mkutano huo alisema, sio tu utakuwa ni chachu katika kuongeza mtangamano na mshikamano baina ya wananchi wa pande zote mbili bali pia utasaidia katika kurahisisha taratibu za kiuhamiaji baina ya raia wa nchi mbii hizo, pamojana kuimamarisha udhibiti wa uhalifu unaovuka mipaka (Transanational Crimes).


Mkutano huo ni mwendelezo wa Mkutano wa tatu wa Wakuu wa Idara za Uhamiaji na Kazi baina ya nchi za Tanzania na Uganda uliofanyika jijini Kampala, Uganda mwezi Novemba mwaka jana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni