Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

05 Novemba 2019

UHAMIAJI YAWAPIGA MSASA MABALOZI WATEULE













Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt Anna Peter Makakala leo ameongoza Ujumbe wa Mabalozi kumi na mbili katika Mafunzo ya huduma mbalimbali za kiuhamiaji zinazotolewa katika Balozi za Tanzania Nje ya Nchi. Mabalozi hao wameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli hivi karibuni.


Katika mafunzo hayo, mada mbalimbali ziliweza kuwasilishwa na Maafisa kutoka Idara ya uhamiaji hususan Pasipoti, Visa za kielektroniki, Huduma za kibalozi (Consular Services) pamoja na Mifumo inayotumika katika utoaji wa Pasipoti na visa za kieletroniki.


Aidha, Waheshimiwa mabalozi walipata fursa ya kutembelea na kujionea namna mifumo mbalimbali ya Uhamiaji inavyofanya kazi na kuonyesha kufurahishwa na jinsi mifumo hiyo inavyorahisisha utoaji wa huduma za uhamiaji kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa.


Kwa upande wake Balozi wa Tanzania Nchini Kuwait, Mheshimiwa Aisha S. Amour kwa niaba ya mabalozi wenzake alimshukuru na Kumpongeza Kamishna Jenerali wa Uhamiaji kwa mafunzo waliyoyapata. Pia ameongeza kuwa, mafunzo hayo yatawajengea uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi hususani katika kuwahudumia Watanzania waishio nje ya nchi na wageni wanaoingia  hapa nchini kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo utalii, matembezi, Biashara na uwekezaji.


Baadhi ya waheshimiwa Mabalozi  waliohudhuria mafunzo hayo ni pamoja na Maj Gen, Gaudence Milanzi, Mohamed A. Mtonga, H.A Kattanga, Aisha S. Amour, Prof. Emmanuel D. Mbennah, Ali J.Mwadini, Dkt. Jilly E. Maleko pamoja na Dkt. Modestus F. Kipilimba.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni