Matangazo
02 Agosti 2018
01 Agosti 2018
WACHEZAJI WA SOKA WA TIMU YA TAIFA UMRI CHINI YA MIAKA 13 WAKABIDHIWA PASI ZAO
Kamishna wa Uhamiaji (Uraia na Pasipoti) Kamishna Gerald Kihinga amekabidhi pasipoti mpya za kielektroniki 16 kwa wachezaji wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Taifa chini ya umri wa miaka 13 (U13) kutoka shule ya Fountain Gate.
Vijana hao wanatarajia kusafiri kwenda nchini Ubelgiji kushiriki mashindano ya Soka ya Dunia kwa vijana wa umri chini ya miaka 13.
Aidha, Kamishna Kihinga aliwapongeza vijana hao kwa kuiwakilisha nchi na kuwataka kucheza kwa juhudi ili walete kombe nchini.
"Leo tumewapatia pasipoti ili muweze kusafiri kwenda kwenye mashindano, pia nawapongeza sana kwa kuchaguliwa kwenu kuiwakilisha nchi yetu, hivyo nawaomba mkacheze kwa juhudi na moyo wa kizalendo ili mchukue kombe na kuiletea sifa nzuri nchi yetu" alisema Kamishna Kihinga.
29 Julai 2018
28 Julai 2018
ASKARI NA MAAFISA UHAMIAJI WAHITIMU MAFUNZO YA UPANDISHWAJI VYEO KATIKA SHULE YA POLISI MOSHI
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali
Jacob Kingu amefunga mafunzo ya upandishwaji vyeo kwa askari na maafisa
uhamiaji yaliyofikia tamati siku ya tarehe 27 Julai 2018. Mafunzo hayo ya miezi
mitatu yaliyofanyika Shule ya Polisi Moshi yalishirikisha askari na maafisa
uhamiaji 507 yalikuwa ni moja ya hatua ya kupanda cheo.
Awali, Meja Jenerali Kingu alikagua vikosi na baadae Gwaride
maalumu la kufunga mafunzo kutoka kwa wahitimu lilipita mbele ya mgeni rasmi
kutoa heshima za ambapo wananchi waliofika kushuhudia sherehe hizo
walishangilia kwa nguvu na vigelegele wakifurahia gwaride hilo.
![]() |
| Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Jacob Kingu akisalimiana na Mkuu wa Shule ya Polisi pamoja na wakufunzi wa shule hiyo. |
![]() |
| Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji cha Kikanda (TRITA) Mrakibu Mwandamizi Bazo akisalimiana na Katibu Mkuu Meja Jenerali Kingu |
![]() |
| Mgeni rasmi Meja Jenerali Kingu na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala (kushoto) wakitoa heshima zao kwa gwaride. |
![]() |
| Gadi ya Askari na Maafisa Uhamiaji likipita mbele ya mgeni Rasmi wakati wa kuhitimisha mafunzo ya Upandishaji vyeo katika shule ya Polisi. |

![]() |
| GAadi ya Askari na Maafisa wa kike ikiongozwa na Mkufunzi Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji Salma Panja likipita mbele ya mgeni rasmi kutoa heshima zake. |
27 Julai 2018
KARIBU NANENANE MKOA WA SIMIYU
Karibu #NaneNane Kitaifa katika Uwanja wa Kanda wa Nyakibindi mjini Bariadi mkoani Simiyu. Kuanzia 01 hadi 08 Agosti 2018. #NaneNane2018
24 Julai 2018
Watumishi wa Uhamiaji waanza Mafunzo ya Usimamizi wa Vihatarishi
Baadhi ya Maafisa Uhamiaji kutoka Ofisi ya Makao Makuu
wameanza mafunzo ya siku tatu juu ya Usimamizi wa Vihatarishi (Risk
Management) katika jengo la Makao Maku ya Idara hiyo Kurasini jijini Dar es
salaam.
Mafunzo hayo yanaratibiwa na Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji
Andrew Malyeta ambaye pia ni Mratibu wa Usimamizi wa Vihatarishi katika Idara hiyo
amesema lengo kuu la mafunzo haya ni kuwapa uelewa watumishi katika Usimamizi wa Vihatarishi kutokana na Muongozo wa Usimamizi wa Vihatarishi
katika Sekta ya Umma (Guidelines for
Developing and Implementing Institutiona Risk Management Framework in Public
Sector, December 2013) pamoja na Sera
ya Usimamizi wa Vihatarishi ya Idara ya Uhamiaji (Institutional Risk Management Framework and Guide for the Immigration
Department, 2016).
“Kwa muongozo na sera hio tunategemea maafisa
wetu watajifunza mambo muhimu sana katika utendaji kazi wao wa kila siku ambayo
ni Muundo wa Usimamizi wa Vihatarishi, Wadau wa Usimamizi wa Vihatarishi,
Majukumu ya mabingwa wa Vihatarishi, Hatua za Usimamizi wa Vihatarishi,
Mgawanyo wa Vihatarishi, rejesta za Viharatishi pamoja na Nyenzo zinazotumika
katika Usimamizi wa Vihatarishi’’ aliongeza Mrakibu Msaidizi
Malyeta.
Mafunzo haya yanafanyika kwa ushirikiano na wawezeshaji
katika Usimamizi wa Vihatarishi kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Bwana
Josephat Kajonga ambaye ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Vihatarishi
na Bi. Lulu Ishengoma ambaye ni Afisa kutoka Kitengo cha Usimamizi wa
Vihatarishi.
Jumla ya Watumishi (askari na kada ya kawaida) 20
wanahudhuria mafunzo haya kutoka vitengo vya Uhasibu, BMC, Manunuzi, Sheria, Mipango,
Anuwai za Jamii na Utumishi.
| Mwezeshaji kutoka NIDA Bw. Josephat Kajonga akielekeza jambo wakati wa Mafunzo hayo. |
| Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamsikiliza muwezeshaji |
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)










