Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

04 Juni 2018

UZINDUZI WA PASIPOTI ZA KIELEKTRONIKI MKOA WA KUSINI PEMBA

Hafla ya Uzinduzi wa Huduma za Pasipoti za Kielekroniki katika ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Kusini Pemba ambayo ilifanyika siku ya tarehe 31/05/2018 ilihudhuriwa na Mgeni Rasmi Mhe. Mohamed Abood, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Katika hafla hiyo ambayo ilihudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba na viongozi mbali mbali wa Serikali ilifanyika katika Ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Kusini Pemba mjini Chakechake.

Mgeni rasmi Mheshimiwa Mohamed Abood katika hotuba yake alisisitiza sana raia kuleta nyaraka sahihi wanapokuja kuomba  pasipoti ili kurahisisha zoezi la utoaji wa pasipoti hizo, kuwataka kuacha kufoji nyaraka ili ili kuepuka kutofautiana kwa taarifa muhimu zinazotakiwa.

Pia alikemea utumaji wa mawakala ambao ni mianya ya rushwa, na watakaogundulika  aidha raia au afisa uhamiaji basi wananchi watoe taarifa kwa Kamishna wa Uhamiaji. Na ikiwa Afisa Uhamiaji anatuhumiwa, Mheshimiwa Abood alimtaka Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Johari Masoud Sururu amsimamishe kazi mara moja na kupisha uchunguzi juu yake.

Mheshimiwa Abood alimaliza kwa kuwataka wananchi wanaopewa pasipoti hizo kuzitunza kwani ikipotea gharama ya kuomba inaongezeka na aliwataka kuzitumia kwa dhumuni husika na sio kuzitupa hovyo.

Hafla hiyo ilimalizika kwa ugawaji wa pasipoti kwa viongozi mbalimbali waliohudhuria.




Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba akionesha pasipoti yake

Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama mkoa wa Kusini Pemba

Mhe. Mohamed Abood akipata maekelezo ya hatua za uchuakuaji wa taarifa za mteja kielekroniki






Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na maafisa na askari wa Uhamiaji wa ofisi ya Mkoa wa Kusini Pemba























Mgeni rasmi akiangalia namna ya uchukuaji wa taarifa za kibaiometriki kwa mteja unavyofanyika







Mwananchi na Mkazi wa Kusini Pemba akikabidhiwa pasipoti yake ya kielektroniki na Mheshimiwa Abood


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni