Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

26 Januari 2021

UHAMIAJI IRINGA YASHIRIKI MAONESHO YA UWEKEZAJI

 Iringa, Tanzania

Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Iringa imeshiriki maonesho ya mwongozo wa uwekezaji mkoa wa Iringa, Maonesho hayo yalifunguliwa tarehe 23 January 2021 na Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) katika viwanja vya maonesho vya chuo kikuu kishiriki cha elimu Mkwawa (MUCE).

Katika maonesho hayo yaliyodumu kwa siku mbili huduma mbalimbali za ki-uhamiaji zilitolewa kama vile ukaguzi na upitishaji wa fomu za vitambulisho vya taifa, elimu ya uraia, elimu juu ya uhamiaji haramu na madhara yake kwa jamii na taifa kwa ujumla sanjari na  kupokea maombi ya passipoti ya kielektroniki n.k.

Maonesho hayo yalijumuisha taasisi za uuma na binafsi zinazotoa huduma katika Mkoa wa Iringa.

HABARI PICHA NA MATUKIO

Elimu ikitolewa





(Picha zote na kitengo cha Uhusiano Uhamiaji Mkoa wa Iringa)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni