Visitors

IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA UHAMIAJI HABARI BLOGU KARIBU KWENYE BLOG RASMI YA IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA TUNAKULETEA MATUKIO YANAYOTOKEA KILA SIKU KATIKA IDARA YA UHAMIAJI TAFADHALI TUNAOMBA TUFUATILIE PIA KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII

01 Februari 2018

TAARIFA KWA UMMA



TAARIFA KWA UMMA:

UFAFANUZI JUU YA “UZUSHI” UNAOENEA KWENYE TOVUTI NA MITANDAO YA KIJAMII KUHUSU IDARA YA UHAMIAJI KUTANGAZA NAFASI ZA KAZI.
Katika siku za hivi karibuni, kumekuwepo na uvumi unaoenezwa kupitia baadhi ya tovuti na mitandao ya kijamii kuhusu kutangazwa kwa nafasi za ajira na Idara ya Uhamiaji kwa ngazi ya Mkaguzi Msaidizi, Koplo na Konstebo. Tunaamini uvumi huo unaenezwa na watu au kikundi cha watu kwa nia ya kujipatia maslahi yao binafsi au kwa malengo wanayoyafahamu wao.

Kufuatia kuwepo kwa taarifa hizo, Idara ya Uhamiaji inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao:
  1. Idara ya Uhamiaji haijatangaza nafasi zozote za ajira katika kipindi cha hivi karibuni, hivyo tunawaomba wananchi wasirubuniwe au kushawishiwa na mtu yoyote kutoa kitu chochote ili waweze kusaidiwa kupata kazi Idara ya Uhamiaji.
  2. Taarifa za kutangazwa nafasi za kazi zilizotolewa kupitia blogu husika na Mitandao ya kijamii si za kweli, bali ni uzushi uliofanywa na watu au kikundi cha watu kwa malengo wanayoyajua wao.

  1. Idara ya Uhamiaji, kama Taasisi ya Serikali hutangaza nafasi za ajira  kwa uwazi kupitia Magazeti, Televisheni na Tovuti yake ambayo niwww.immigration.go.tz

  1. Idara inalaani na kukemea vikali watu au kikundi cha watu kinachotoa taarifa za upotoshaji kuhusu Idara kutangaza nafasi za kazi kama ambavyo imeripotiwa kwenye baadhi ya tovuti na mitandao ya kijamii.

Imetolewa na;
KITENGO CHA UHUSIANO,
MAKAO MAKUU, DAR ES SALAAM.
TAREHE: 01 FEBRUARI, 2018

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni